Amosi 5:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
6 Mutafute Yawe, nanyi mutaishi! Kama sivyo, atawatokea wazao wa Yosefu kama moto; moto utawateketeza wakaaji wa Beteli na hakuna mutu atakayeweza kuuzimisha.
Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?
Nitawaimarisha watu wa Yuda; nitawaokoa wazao wa Yosefu. Nitawarudisha kwao kwa maana ninawaonea huruma, nao watakuwa kama vile sikuwa nimewakataa. Mimi ni Yawe, Mungu wao, nami nitayasikiliza maombi yao.
Wewe utawajibu: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakitwaa kijiti cha Yosefu (kinachokuwa katika mukono wa Efuraimu) na makabila ya Israeli yanayoungana naye, nami nitakishikamanisha na kijiti cha Yuda kusudi vijiti hivyo viwili vifanywe kijiti kimoja katika mukono wangu.
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaimwanga hasira yangu juu ya pahali hapa, juu ya wanadamu na nyama, miti katika mashamba na juu ya mazao ya inchi. Nayo nafasi hii itawaka moto wala hautaweza kuzimishwa.
Enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema, mujitahiri, mukiondoa govi za mioyo yenu, mupate kujitoa kwa Yawe. Kama si vile, kasirani yangu itawaka kama moto, nayo itaunguza wala hakuna atakayeizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.
Wenye nguvu watakuwa kama majani yenye kukauka, matendo yao yatakuwa kama cheche za moto. Watateketea pamoja na matendo yao, wala hakutakuwa mutu wa kuwaokoa.
Yeroboamu alionekana kuwa kijana hodari na shujaa. Wakati Solomono alipoona kwamba huyo kijana alikuwa mwenye bidii, akamuweka akuwe musimamizi wa kazi za kulazimishwa zilizofanywa na watu wa ukoo wa Yosefu.
Simei akamwambia mufalme: “Ninakuomba, bwana wangu mufalme, usinihesabu kuwa na kosa wala kukumbuka kosa nililofanya siku ile ulipokuwa ukiondoka Yerusalema. Ninakuomba usiyaweke hayo ndani ya moyo.
Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.
Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.
Kwa sababu wameniacha mimi na kufukizia miungu mingine ubani kusudi wanikasirikishe sana kwa kazi zote za mikono yao, basi kasirani yangu itamwagika juu ya pahali hapa wala haitatulizwa.
Yeremia akamujibu: Hautatolewa kwao. Wewe sasa utii kile Yawe anachosema, kama ninavyokuambia, na mambo yote yatakuendekea vema, na maisha yako yataokolewa.
Uwaambie wasikilize neno la Yawe. Uwaambie kwamba Bwana wao Yawe anasema hivi: Nitawasha moto kwako, nao utateketeza miti yote, mibichi na yenye kukauka; utaenea tangu kusini mpaka kaskazini wala hakuna atakayeweza kuzimisha ndimi zake. Nao utaunguza watu wote.