Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kwa hiyo, enyi Waisraeli, nitawaazibu. Na kwa sababu nitafanya jambo lile, mujitayarishe kwa kutana na Mungu wenu!

Gade chapit la Kopi




Amosi 4:12
20 Referans Kwoze  

Hawakwenda kulinda sehemu zile za kuta zilizobomoka wala hawajengi kuta mupya kusudi Waisraeli waweze kujilinda wakati wa vita siku ile ambayo mimi Yawe nimeiweka.


Watu watauona uchi wako; wataona haya yako. Mimi nitalipiza kisasi, wala sitamuhurumia mutu yeyote.


Kwa hiyo, ninyi vilevile mukuwe tayari, kwa sababu Mwana wa Mutu atarudi saa musiyozania.


“Kama mutu akikushitaki, upatane naye upesi wakati mungali katika njia kwenda kwenye tribinali. Kama si vile, yule anayekushitaki atakutoa kwa mwamuzi, naye mwamuzi atakupeleka kwa askari, nawe utatupwa katika kifungo.


Nitawarukia kama dubu aliyenyanganywa watoto wake. Nitawararua vifua vyenu na kuwakula palepale kama simba; nitawararua vipandevipande kama nyama wa pori.


Nilitafuta kati yao mutu mumoja atengeneze ukuta na kusimama juu ya nafasi iliyobomoka mbele yangu, kusudi ailinde inchi na kunizuia nisiiharibu, lakini sikumupata hata mumoja.


Basi ukumbuke mafundisho uliyopokea na yale uliyosikia. Uyashike na kugeuka toka zambi zako. Kama usipokesha, nitakuja kama mwizi, wala hautajua saa nitakapokuja kwako.


Hata wale wenye kuwa hodari kwa kukimbia mbio hawataweza kutoroka; wenye nguvu wataishiwa nguvu zao, na waaskari watashindwa kuyaokoa maisha yao.


Mutetemeke kwa woga, enyi munaojiikalia tu; mutetemeke kwa hofu, enyi munaostarehe! Muvue nguo zenu, mubakie uchi, mujifungie nguo ya gunia katika viuno vyenu.


Wakati ulipotenda maajabu ambayo hatukutazamia, ulishuka chini nayo milima ikatetemeka ilipokuona.


Mbona hamuniogopi? –Ni ujumbe wa Yawe.– Kwa nini hamutetemeki mbele yangu? Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake; ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka. Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita; ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite