Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:

Gade chapit la Kopi




Amosi 4:1
49 Referans Kwoze  

Usikae mbali nami, kwa maana taabu imekaribia; wala hakuna wa kunisaidia.


Ole kwenu ninyi munaostarehe kule Sayuni, nanyi munaoishi katika usalama kwenye mulima Samaria! Ninyi munaonekana kuwa waongozi wa taifa kubwa, ambao Waisraeli wote wanawategemea.


Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake.


Watakula nyama ya mashujaa, watakunywa damu ya wakubwa wa dunia watakaochinjwa kama kondoo dume au wana-kondoo, mabeberu au ngombe dume wanono wa Basani.


Kisha nikaona mateso yote yanayofanyika chini ya jua. Watu wanaogandamizwa wanalia machozi, lakini hakuna mutu yeyote anayewafariji. Wagandamizaji wao wana nguvu, ndiyo sababu hakuna wa kuwafariji.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Nitafanya kitambulisho cha ajabu mbinguni na katika dunia; kutakuwa damu, moto na minara ya moshi.


Kila fasi katika inchi watu wanatendeana vibaya na kunyanganya kwa kinguvu. Wanagandamiza wamasikini na wakosefu, na kuwaonea wageni bila kujali.


Wakubwa wake wanaokuwa ndani ya muji ni kama imbwa wa pori wanaorarua nyama wao; wanaua kwa kujitajirisha kwa namna isiyokuwa ya haki.


Huko kwako kuna watu ambao wanapokea kitulizo kwa kumwanga damu. Wanakopesha kwa kudai faida ya juu, wananyanganya mali za wenzao kwa nguvu, na kunisahau mimi kabisa! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Kwako baba na mama wanazarauliwa. Mugeni anayekaa kwako ananyanganywa mali yake. Wayatima na wajane wanaonewa.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli aliuharibu na kuuponda Yerusalema aliuacha kama chungu kitupu; aliumeza kama vile nyoka mukubwa. Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri, akautupilia mbali kama matapiko.


Muwaue waaskari wake hodari; muache washukie kwenye machinjo. Ole kwao, maana siku yao imetimia, wakati wao wa kuazibiwa umefika!


Musiwatese wageni, wayatima au wajane au kuwaua watu wasiokuwa na kosa katika inchi hii. Musijiangamize wenyewe kwa kuabudu miungu mingine.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mukate miti na kulundika udongo, kwa kuweza kupandia ndani ya Yerusalema. Muji huu unapaswa uazibiwe, maana hamuna lolote ndani yake isipokuwa ukorofi tu.


Mafungo ninayotaka mimi ni haya: kuwafungua waliofungwa bila haki, kuziondoa kamba za utumwa, kuwaacha huru wanaogandamizwa, na kuvunja kabisa mambo yote ya kitumwa!


Ole kwao wanaoongeza nyumba juu ya nyumba, wanaoongeza mashamba juu ya mashamba yao, mpaka kila sehemu inakuwa mali yao, na hakuna nafasi kwa wengine katika inchi.


Faida ya mavuno ya inchi ni kwa watu wote, hata mufalme vilevile anatumainia mavuno yale.


Wanaosingizia wengine wasifanikiwe katika inchi; uovu uwapate watesaji wakali na kuwaangamiza bila kukawia!


Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”


kwa sababu amewaangamiza wamasikini na kuwaachilia, amenyanganya nyumba ambazo hakuzijenga.


Alinunua mulima wa Samaria kwa vikoroti elfu sita vya feza kutoka kwa mutu mumoja anayeitwa Semeri, akajenga muji wenye kuta juu yake. Muji wenyewe akauita Samaria, kwa heshima ya Semeri aliyekuwa mwenyeji wa mulima huo hapo zamani.


“Taifa musilolijua litatwaa mazao yote ya inchi yenu na matunda ya jasho lenu, nanyi mutapondwa na kuteswa siku zote,


Enyi wanyanganyi wa mali yangu, ijapokuwa munafurahi na kushangilia, munarukaruka kama mwana-ngombe anayepepeta ngano, na kulia kama farasi dume,


“Usimutese mutumishi wako wa mushahara anayekuwa masikini na muhitaji, akuwe Mwisraeli au mumoja wa wageni wanaoishi katika miji yenu.


Munakunywa divai katika mabakuli, na kujipakaa marasi mazuri kabisa. Lakini hamuhuzuniki hata kidogo juu ya kuangamia kwa wazao wa Yosefu.


Waisraeli wakageuka wakafuata njia inayoenda Basani. Mufalme Ogi wa Basani akatoka na jeshi lake kwa kuwashambulia huko Edirei.


Wanasukuma wamasikini kandokando ya barabara; wamasikini wa dunia wanajificha mbele yao.


Tajiri anamutawala masikini. Mwenye kukopesha ni mutumwa wa mwenye kukopeshwa.


Ole wa Samaria, muji unaokuwa kama taji juu ya bonde kwenye udongo muzuri. Walevi wa ajabu wa Efuraimu wanajivuna kwa ajili yake, lakini utukufu wake utatoweka kama ua linalonyauka!


Wao wanaambiana hivi: Mukuje, tuende kutafuta divai; mukuje tukunywe tushibe kinywaji kikali! Kesho itakuwa kama leo, tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.


Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.


Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:


Watu wawili wanaweza kusafiri pamoja bila kupatana kwanza?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite