Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mutangaze katika nyumba nzuri kule Asidodi, na katika nyumba nzuri za inchi ya Misri: Mukusanyike kwenye milima inayoizunguka inchi ya Samaria, mujionee fujo kubwa na mateso yanayofanyika kule.

Gade chapit la Kopi




Amosi 3:9
22 Referans Kwoze  

Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Ole kwenu ninyi munaostarehe kule Sayuni, nanyi munaoishi katika usalama kwenye mulima Samaria! Ninyi munaonekana kuwa waongozi wa taifa kubwa, ambao Waisraeli wote wanawategemea.


Nitaondoa wakaaji wa muji wa Asidodi, pamoja na mutawala wa Asikeloni. Nitanyoosha mukono wangu kwa kuazibu muji wa Ekuroni, na Wafilistini wote waliobaki wataangamia. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Tutawanunua wamasikini kwa feza na wakosefu kwa bei ya muguu mumoja wa mapapa. Nasi tutauzisha machenga ya ngano.


Mutangaze kati ya mataifa, munyanyue bendera na kutangaza, musifiche jambo lolote. Museme: Babeli umetekwa, mungu Beli amepatishwa haya. Merodaki amefazaishwa; sanamu zake zimefezeheshwa, miungu yake imefazaishwa.


Utapanda tena mizabibu juu ya milima ya Samaria; walimaji watapanda mbegu na kuyafurahia mazao yake!


Nyuma ya Wafilistini kuliteka Sanduku la Mungu, walilibeba kutoka muji wa Ebeni-Ezeri mpaka katika muji wao wa Asidodi.


Nitawafanya kuwa taifa moja katika inchi juu ya milima ya Israeli; mufalme mumoja atakuwa mufalme wao wote. Hawatakuwa tena mataifa mawili wala hawatagawanyika tena kuwa falme mbili.


Lakini juu ya milima ya Waisraeli, miti itatoa matawi na kuzaa matunda kwa ajili ya watu wangu Waisraeli, maana wao wanakaribia kurudi katika inchi yao.


Tangaza katika inchi ya Misri, uijulishe huko Migidoli, uijulishe huko Nofi na Tapanesi. Uwaambie: Mukae tayari kabisa maana upanga utawaangamiza kila nafasi.


Musiuambie muji wa Gati jambo lile wala katika barabara za Askeloni, kusudi wanawake wa Wafilistini wasishangilie, wabinti za wapagani wasifurahi.


Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake.


Tutajitwalia mali zote za bei kali, tutazijaza nyumba zetu vitu tulivyonyanganya.


Mwanamuke mwema anaheshimiwa; wanaume wenye nguvu wanatajirika.


Kisha nikaona mateso yote yanayofanyika chini ya jua. Watu wanaogandamizwa wanalia machozi, lakini hakuna mutu yeyote anayewafariji. Wagandamizaji wao wana nguvu, ndiyo sababu hakuna wa kuwafariji.


Kila mara nikitaka kurudishia watu wangu hali yao ya mbele, ninapotaka kuwaponyesha Waisraeli, uovu wa watu wa Efuraimu unafunuliwa, matendo mabaya ya Samaria yanajitokeza. Wao wanaongozwa na udanganyifu, mwizi anabomoa nyumba; inje katika barabara wanyanganyi wanashambulia.


Ninyi munajaribu kuifukuza ile siku mbaya. Lakini munaukaribisha utawala wa mateso.


Nitavumilia maovu yaliyolundikwa ndani ya nyumba yao, mali zilizopatikana kwa udanganyifu, na matumizi ya vipimo vya udanganyifu, jambo ambalo ni chukizo?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite