Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 3:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Baragumu ya vita inalia katika muji bila kutia watu hofu? Muji unaweza kupatwa na hasara ambayo haikuletwa na Mungu?

Gade chapit la Kopi




Amosi 3:6
17 Referans Kwoze  

Mimi ninafanya mwangaza na kuumba giza; ninaleta uheri na kusababisha hasara. Mimi Yawe ninatenda vitu hivi vyote.


Siku hiyo ni ya mulio wa baragumu ya vita, juu ya miji yenye vikingio na kuta ndefu.


Basi, kwa sababu tunajua kwamba ni lazima kumwogopa Bwana, ndiyo maana tunajitoa kuwavuta watu kwake. Mungu anatujua waziwazi nami ninatumaini kwamba ninyi wenyewe munatujua waziwazi vilevile.


Ninyi mulitaka kunitendea vibaya, lakini Mungu alikusudia mema kusudi watu wengi wapate kuwa wazima kama vile munavyoona leo.


Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.


Enyi watu wa kabila la Benjamina, muondoke Yerusalema, mukimbie! Mupige baragumu katika muji Tekoa! Muonyeshe kitambulisho cha vita huko Beti-Keremu, maana hasara na maangamizi makubwa vinakuja kutoka upande wa kaskazini.


Mutoe tangazo, mupashe habari huko Yerusalema! Mupige baragumu kila pahali katika inchi! Mulalamike, mukisema: Mukusanyike pamoja! Mukimbilie katika miji yenye kuzungukwa na kuta!


Hivi walitimiza mambo uliyokuwa umekusudia tangu zamani kwa uwezo wako na kwa mapenzi yako.


huyo anapoona waadui wanakuja, atapiga baragumu na kuwaonya watu.


Nani asiyekuogopa wewe, ee mufalme wa mataifa? Wewe unastahili kuheshimiwa: kwa maana kati ya wenye hekima wote wa mataifa, na katika falme zao zote, hakuna hata mumoja anayekuwa kama wewe.


Mupige baragumu kule Gibea, na ngunga kule Rama. Mupige kelele la kujulisha hatari kule Beti-Aweni. Enyi watu wa Benjamina, adui yenu yuko nyuma!


Mbona hamuniogopi? –Ni ujumbe wa Yawe.– Kwa nini hamutetemeki mbele yangu? Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake; ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka. Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita; ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.


Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.


Mutego bila chambo utamunasa ndege? Mutego unaweza kufyatuka bila kuguswa na kitu?


Mbele ya wakati huo, watu hawakupata mushahara kwa kazi zao wala mali kwa ajili ya kutumikisha nyama. Hamukuwa na usalama kwa sababu ya waadui zenu, maana nilisababisha uadui kati ya watu wote.


Mbele hata hajamaliza kusema, mufalme akafika, akasema: “Mabaya haya yametoka kwa Yawe! Nitangojea nini tena kutoka kwake?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite