Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:

Gade chapit la Kopi




Amosi 3:1
18 Referans Kwoze  

Niliwatoa ninyi kutoka inchi ya Misri, nikawaongoza kupitia katika jangwa miaka makumi ine, mpaka mukaitwaa inchi ya Waamori kuwa yenu.


Sasa musikilize, enyi wakubwa wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa wazao wa Israeli! Ninyi ndio munaopaswa kujua namna ya kufuata sheria ya Mungu.


Watu wote watakaobaki wa jamaa hii mbaya, pahali popote pale nilipowasambaza, wataona heri kufa kuliko kuishi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Musikilize maneno ya Yawe, enyi Waisraeli. Yawe anawashitaki wakaaji wa inchi hii. Hakuna tena uaminifu wala wema katika inchi; hakuna anayemujua Mungu katika inchi hii.


Kutakuja siku ambazo nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Waisraeli, nao watakuwa watu wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Unisikilize ee taifa la Yakobo, unisikilize ee Israeli niliyekuita. Mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


Yahazieli akasema: “Musikilize ninyi watu wa Yuda na wakajii wa Yerusalema na mufalme Yosafati, Yawe anawaambia hivi: musiogope wala musihangaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Vita hivi si vyenu, lakini ni vya Mungu.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa!


Musikilize, enyi makuhani! Mutege sikio, enyi Waisraeli! Musikilize, enyi ukoo wa kifalme! Ninyi mulipaswa kulinda haki, pahali pake mumekuwa kama mutego kule Misipa, mumekuwa kama wavu wa kuwanasa kule Tabori.


Musikilize, enyi wazao wa Yakobo, munisikilize, enyi mabaki ya watu wangu wa Israeli. Mimi niliwatunza ninyi tangu mulipozaliwa; niliwabeba ninyi tangu katika tumbo la mama yenu.


Kama vile mukaba unavyoshikamana na kiuno cha mutu, ndivyo nilivyowashikamanisha nami watu wa Israeli na watu wa Yuda, kusudi wajulikane kwa jina langu, wanisifu na kunitukuza. Lakini wao hawakunisikiliza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninapanga kuwaletea ninyi hasara, ambayo hamutaweza kuiponyoka hata kidogo. Utakuwa wakati mubaya kwenu, wala hamutaweza kutembea kwa maringo.


Ole wenu wakaaji wa inchi za pembeni ya bahari, watu wanaoishi kule Krete! Yawe amesema juu yenu, enyi wakaaji wa Kanana, inchi ya Wafilistini: Mimi nitawaangamiza wala hakutabaki hata mukaaji mumoja!


enyi wazao wa Abrahamu, mutumishi wake, enyi wazao wa Yakobo, wachaguliwa wake.


Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Musikilize maombolezo yangu juu yenu, enyi Waisraeli:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite