Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Juu ya kila mazabahu, watu wanalalia nguo walizozitwaa kwa masikini kama rehani ya madeni yao; na katika nyumba ya Mungu wao, wanakunywa divai waliyotwaa kwa wenye kuwa na madeni yao.

Gade chapit la Kopi




Amosi 2:8
17 Referans Kwoze  

Munakunywa divai katika mabakuli, na kujipakaa marasi mazuri kabisa. Lakini hamuhuzuniki hata kidogo juu ya kuangamia kwa wazao wa Yosefu.


Hamuwezi kuchangia kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo. Vilevile hamuwezi kuchangia meza ya Bwana na meza ya pepo.


Basi musikuwe wenye kuabudu sanamu kama wamoja kati yao walivyokuwa; kama vile Maandiko haya Matakatifu yanavyosema: “Watu wakaikaa kula na kunywa na kisha wakasimama kwa kujifurahisha.”


Kwa maana kama mutu zaifu katika imani akikuona wewe mwenye elimu unakula katika hekalu la sanamu, si zamiri yake itamusukuma kula vyakula vya kutambikia sanamu?


Ole kwenu ninyi munaolalia juu ya vitanda vya pembe za tembo na kujinyoosha juu ya matandiko yao, mukikula nyama za wana-kondoo na wana-ngombe!


Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Wanajishibisha kwa sadaka za watu wangu wenye zambi. Wana hamu sana ya kuwaona wakitenda zambi.


Kisha wakaikaa kwenye vitanda vizurivizuri, na mbele yao meza imetandikwa. Juu ya meza hiyo uliweka ubani wangu na mafuta yangu.


Wakatoka na kwenda kwenye mashamba yao ya mizabibu, wakachuma zabibu halafu wakazikamua, wakatengeneza divai wakafanya sikukuu. Wakaingia kwenye nyumba ya mungu wao wakakula na kunywa, kisha wakamutukana Abimeleki.


Mumeweka vitanda vyenu juu ya milima mirefu, na kwenda kule kwa kutambikia.


Wananililia, lakini si kwa moyo. Wanagaagaa na kujikatakata juu ya vitanda vyao, kusudi nisikilize maombi yao kwa kupata ngano na divai; lakini wanaendelea kuniasi.


Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.


Ukitwaa nguo ya mwenzako kama rehani, lazima umurudishie mbele ya jua kutua,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite