Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Ninyi muliwakunywesha wanaziri divai, na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.

Gade chapit la Kopi




Amosi 2:12
8 Referans Kwoze  

Usitoe tena unabii hapa katika Beteli, kwa sababu hapa ni pahali ya ibada ya mufalme; ni hekalu la utawala huu.


Wanawaambia wale wanaopata maono hivi: Musipate maono. Wanawaambia manabii hivi: Musitutangazie ukweli, lakini mutuambie mambo ya kupendeza, mutoe unabii wa mambo ya udanganyifu tu.


Usituhubirie sisi. Mambo kama hayo si ya kuhubiriwa. Sisi hatutapatwa na hasara!


Kwa hiyo Yawe wa majeshi anasema hivi juu ya watu wa Anatoti ambao wanataka kuniua na kuniambia: Usitutabirie kwa jina la Yawe, kama si vile tutakuua.


Nawe basi, ewe Amazia, sikiliza neno la Yawe: Wewe unaniambia nisitoe unabii juu ya Waisraeli, wala nisiseme neno lolote juu ya wazao wa Isaka.


Uwape Waisraeli maagizo haya: Ikiwa mwanaume au mwanamuke atafanya kiapo kuwa munaziri, ni kusema kujitenga kwa ajili ya Yawe,


Kisha nikaleta vikombe na mabakuli yaliyojaa divai mbele ya hao Warekabu, nikawaambia: Mukunywe divai.


basi, asikunywe divai au kileo, asikunywe siki ya divai au ya namna nyingine, asikunywe maji ya zabibu wala kula zabibu zilizoiva au kavu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite