Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Tiro, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka mpaka Edomu. Hawakutii mapatano ya urafiki waliokuwa wamefanya.

Gade chapit la Kopi




Amosi 1:9
23 Referans Kwoze  

Kisha, mufalme Hiramu wa Tiro alituma wajumbe kwa Daudi. Alimupelekea vilevile miti ya mierezi, waseremala na wajengaji ambao walimujengea Daudi nyumba ya kifalme.


“Ole kwako, muji Korazini! Ole kwako, muji Betesaida! Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yenu ingalifanyika katika muji wa Tiro na muji wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuvaa magunia na kujipakaa majivu, kwa kuonyesha kwamba wamegeuka toka zambi zao.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Edomu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamewawinda wandugu zao Waisraeli kwa mapanga, wakaitupilia mbali huruma yao yote ya kindugu. Hasira yao haikuwa na mwisho, waliiacha iwake siku zote.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Gaza, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka kwa Waedomu.


Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilistini wote, kukomesha musaada uliobakia kutoka Tiro na Sidona. Maana Yawe anawaangamiza Wafilistini, watu waliobaki wa kisanga cha Kafutori.


wafalme wote wa Tiro na Sidona; wafalme wa inchi zinazokuwa kandokando ya bahari ya Mediteranea;


Kwa hiyo ninawaambia kwamba kwa Siku ya hukumu, ninyi mutaazibiwa zaidi kuliko muji wa Tiro na wa Sidona.


Yesu akaendelea kusema: “Ole kwako muji Korazini! Ole kwako muji Betesaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika ndani yenu ingefanyika katika muji wa Tiro na wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuonyesha masikitiko yao kwa kuvaa magunia na kujipakaa majivu, na kugeuka toka zambi zao.


Kwa hiyo, Siku ile ya hukumu, mutaazibiwa vikali zaidi kuliko Tiro na Sidona.


Waedomu na Waisimaeli, Wamoabu na Wahagari;


Kwa wingi wa mabaya yako na udanganyifu katika biashara yako ulipachafua pahali pako pa kuabudia; kwa hiyo niliwasha moto kwako, nao ukakuteketeza, nami nikakufanya kuwa majivu juu ya inchi, mbele ya wote waliokuangalia.


Siku ile mulisimama pembeni mukiangalia tu, wakati wageni walipouteka utajiri wao, walipoingia katika milango yake na kugawanya utajiri wa Yerusalema kwa kupiga kura. Nanyi vilevile mulikuwa kama wamoja wao.


Ujumbe wa Yawe: Neno la Yawe ni juu ya azabu ya miji Hadiraki na Damasiki. Maana inchi ya Aramu ni mali ya Yawe, kama vile makabila yote ya Israeli yanavyokuwa,


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Mali yako, biashara yako, na vitu vyako, waongozi wako wote katika chombo, wafundi wako wa mashua na wachuuzi wako, waaskari wako wote wanaokuwa kwako, pamoja na wasafiri wanaokuwa kwako, vyote vitaangamia ndani ya bahari, siku ile ya kuangamizwa kwako.


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite