Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Nitaondoa wakaaji wa muji wa Asidodi, pamoja na mutawala wa Asikeloni. Nitanyoosha mukono wangu kwa kuazibu muji wa Ekuroni, na Wafilistini wote waliobaki wataangamia. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.

Gade chapit la Kopi




Amosi 1:8
17 Referans Kwoze  

basi, mimi Bwana wenu Yawe ninawaambia hivi: Nitanyoosha mukono juu ya Wafilistini kwa kuwaazibu; nitawaangamiza hao watu wa Kereti na wakaaji wa kandokando ya bahari.


Muji wa Asidodi utakaliwa na wana haramu. Yawe anasema hivi: Nitakikomesha kiburi cha Wafilistini.


Sargoni, mufalme wa Asuria, alimutuma jemadari wake mukubwa kushambulia muji wa Asidodi. Naye akaushambulia na kuuteka.


Heri watu wangu wangenisikiliza! Heri Israeli angefuata njia zangu!


Uzia akaondoka kwa kupigana vita na Wafilistini, akabomoa kuta za miji ya Gati, Yabune na Asidodi. Akajenga miji katika eneo la Asidodi na fasi ingine katika inchi ya Filistia.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Mutangaze katika nyumba nzuri kule Asidodi, na katika nyumba nzuri za inchi ya Misri: Mukusanyike kwenye milima inayoizunguka inchi ya Samaria, mujionee fujo kubwa na mateso yanayofanyika kule.


Nitapigana nawe; nitayeyusha uchafu wako kabisa, na kuondoa takataka yako yote.


Hili ni neno Yawe alilomwambia nabii Yeremia juu ya Wafilistini, mbele mufalme wa Misri hajaushambulia muji wa Gaza:


Jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Yawe, siku inayokuwa kubwa na ya kutisha.


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Gaza, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri.


Wazao wa Yakobo watakuwa kama moto na wazao wa Yosefu kama ndimi za moto. Watawaangamiza wazao wa Esau kama vile moto unavyoteketeza majani yenye kukauka, hakutaponyoka hata mumoja wao. –Yawe amesema.


Muji wa Askeloni utaona hayo na kuogopa, nao muji wa Gaza utagaagaa kwa uchungu; hata Ekroni, maana tumaini lake litatoweka. Gaza utapoteza mufalme wake, nao Askeloni hautakaliwa na watu.


Wafilistini walizipeleka zile sanamu tano za zahabu na za majipu kwa Yawe zikiwa sadaka ya malipo ya makosa yao, sanamu moja kwa ajili ya muji mumoja, muji wa Asidodi, muji wa Gaza, muji wa Asikeloni, muji wa Gati na kwa muji wa Ekuroni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite