Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Gaza, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka kwa Waedomu.

Gade chapit la Kopi




Amosi 1:6
18 Referans Kwoze  

Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Edomu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamewawinda wandugu zao Waisraeli kwa mapanga, wakaitupilia mbali huruma yao yote ya kindugu. Hasira yao haikuwa na mwisho, waliiacha iwake siku zote.


Wakati uleule, Wafilistini walikuwa wakiishambulia miji ya Sefela na Negebu ya Yuda. Walinyanganya miji ya Beti-Semesi, Ayaloni, Gederoti, Soko na vijiji vyake, Timuna na vijiji vyake, Gimuzo na vijiji vyake, wakafanya makao yao kule.


Siku ile mulisimama pembeni mukiangalia tu, wakati wageni walipouteka utajiri wao, walipoingia katika milango yake na kugawanya utajiri wa Yerusalema kwa kupiga kura. Nanyi vilevile mulikuwa kama wamoja wao.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Tiro, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka mpaka Edomu. Hawakutii mapatano ya urafiki waliokuwa wamefanya.


Wafilistini walizipeleka zile sanamu tano za zahabu na za majipu kwa Yawe zikiwa sadaka ya malipo ya makosa yao, sanamu moja kwa ajili ya muji mumoja, muji wa Asidodi, muji wa Gaza, muji wa Asikeloni, muji wa Gati na kwa muji wa Ekuroni.


Ulikuwa adui wa siku zote wa Waisraeli, ukasababisha watu wake wauawe kwa upanga, wakati wa musiba wao, wakati wa azabu yao ya mwisho.


Muji wa Askeloni utaona hayo na kuogopa, nao muji wa Gaza utagaagaa kwa uchungu; hata Ekroni, maana tumaini lake litatoweka. Gaza utapoteza mufalme wake, nao Askeloni hautakaliwa na watu.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Damasiki, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekatakata watu wa Gileadi wakitumia majembe ya mashini ya kulima.


Hili ni neno Yawe alilomwambia nabii Yeremia juu ya Wafilistini, mbele mufalme wa Misri hajaushambulia muji wa Gaza:


Malaika wa Bwana akamwambia Filipo: “Ujitayarishe na uende upande wa kusini kupitia njia inayotelemuka toka Yerusalema kwenda katika muji Gaza, nayo ni njia watu wasiyozoea kupitia.”


Jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Yawe, siku inayokuwa kubwa na ya kutisha.


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Gaza, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite