Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Amosi 1:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Raba, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri. Siku hiyo ya vita kutakuwa makelele mengi, nayo mapambano yatakuwa makali kama zoruba.

Gade chapit la Kopi




Amosi 1:14
20 Referans Kwoze  

Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Moabu, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za muji wa Kerioti. Waaskari watakapolalamika kwa sauti zao na kupiga baragumu, watu wa Moabu watakufa katika makelele hayo ya vita.


Kwa hiyo, siku zinakuja ambapo nitavumisha sauti ya vita juu ya Raba muji wa Waamoni. –Ni ujumbe wa Yawe.– Raba utakuwa lundo la uharibifu, vijiji vyake vitateketezwa kwa moto. Halafu Israeli atatwaa tena urizi wake. Ni Yawe anayesema hivyo.


(Mufalme Ogi ndiye peke yake aliyebakia kati ya Warefai. Kitanda chake kilichotengenezwa kwa chuma, kilikuwa na urefu wa metre ine na upana wa karibu metre mbili. Kitanda hicho kipo katika muji wa Waamori wa Raba.)


Yawe atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa ndimi za moto mukali, ngurumo, zoruba na mvua ya mawe.


Wakati ule, Yoabu aliushambulia Raba muji wa Waamoni, naye akauteka muji ule wa kifalme.


Nami niliwatawanya kwa upepo mukali kati ya mataifa yote ambayo hawakuyajua. Hivyo inchi waliyoiacha ikabaki tupu; hapakuwa mutu yeyote aliyekaa mule; inchi hiyo ya kupendeza ikakuwa ukiwa.


Wakati wa mwisho mufalme wa kusini atamushambulia mufalme huyo wa kaskazini. Lakini mufalme wa kaskazini atajibu mashambulio hayo kwa nguvu kama zoruba, akitumia magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na mashua nyingi. Atashambulia inchi nyingi na kupita katika inchi hizo kama mafuriko ya maji.


Nitaufanya muji wa Raba kuwa nafasi ya kukulishia ngamia na inchi ya Amoni kuwa zizi la kondoo. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Maana mutoto amezaliwa kwa ajili yetu, tumepewa mutoto mwanaume. Naye atapewa mamlaka ya kutawala. Ataitwa: “Mushauri wa Ajabu”, “Mungu Mwenye Nguvu”, “Baba wa Milele”, “Mufalme wa Amani”.


Kama vile moto unavyoteketeza pori, na ndimi za moto zinavyounguza milima,


Kila mara baragumu inapopigwa, yeye anatoa sauti; anasikia harufu ya vita toka mbali, anasikia mushindo wa majemadari wakitoa amri kwa makelele.


Ilipokuwa kwa mwanzo wa mwaka mupya, wakati ambapo wafalme wanaenda kwa vita, Daudi alimutuma Yoabu na wakubwa wake pamoja na waaskari wote wa Israeli kupigana. Nao waliteka Waamoni na kushambulia muji wa Raba. Lakini Daudi alibaki Yerusalema.


Ilipokuwa wakati wa kipwa, wakati ambapo wafalme wanaenda kwa vita, Yoabu akaongoza jeshi na kuharibu inchi ya Waamoni, akaenda vilevile na kuzunguka muji wa Raba kwa vita. Lakini Daudi alibaki kule Yerusalema. Naye Yoabu akashambulia muji wa Raba na kuuteka.


Yawe wa majeshi atakuja kukusaidia; atakuja na ngurumo, tetemeko la inchi na sauti kubwa; atakuja na upepo mukali, zoruba na moto wenye kuunguza.


Angalia, zoruba kali kutoka kwa Yawe; kasirani yake imeamuka, upepo mukali utapiga kichwa cha mwovu.


Kwa hiyo wamevunjika moyo na wengi wanaanguka. Nimeiweka chongo ya upanga katika milango yao yote. Umefanywa uangae kama umeme, umengarishwa kwa ajili ya mauaji.


Nami nitapiga mikono, kasirani yangu itatosheka. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


basi, mimi nimeunyoosha mukono juu yenu kwa kuwaazibu; nitawaacha mukamatwe mateka na watu wa mataifa mengine. Nitawaangamiza kabisa, nanyi hamutakuwa taifa tena wala kuwa na inchi. Kwa hiyo mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Halafu aliwakamata watu wa muji ule, akawaweka kwa kazi ya kutumikisha misumeno, sururu za chuma, mashoka ya chuma na kuwatumia kufanya kazi katika furu ya matofali. Hivi ndivyo alivyoitendea miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na watu wote walirudi Yerusalema.


Utachora njia upanga utakapopitia kwenda kuufikilia muji Raba wa Waamoni, na njia ingine inayoelekea Yerusalema wenye kuzungukwa na kuta katika inchi ya Yuda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite