Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Wakorinto 8:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ninayashuhudia kwamba kwa mapenzi yao yalitoa kwa kadiri yalivyoweza na hata zaidi kupita uwezo wao.

Gade chapit la Kopi




2 Wakorinto 8:3
22 Referans Kwoze  

Waisraeli wote, wanaume na wanawake, ambao walivutwa ndani ya moyo wao kuleta kitu chochote kwa ajili ya kazi ambayo Yawe alikuwa amemwagiza Musa ifanyike, walileta vitu hivyo kwa mapenzi yao, kama vile muchango wa kumupa Yawe.


Mutatoa katika mali zenu muchango wa kumupa Yawe. Kila mutu mwenye moyo mwema atamuletea Yawe muchango: sadaka, feza, shaba;


Lakini sikutaka kufanya kitu chochote pasipo shauri lako. Wala sikutaka kukulazimisha unitendee mema; lakini ningetaka uyatende kwa mapenzi yako mwenyewe.


Kila siku ya kwanza ya juma, kila mumoja wenu anapaswa kuweka akiba ya mali kwake, kwa kadiri ya mapato yake, kusudi musihitaji kufanya muchango wakati nitakapokuja.


Wanafunzi wakakusudia kutuma musaada kwa wandugu waamini waliokaa katika jimbo la Yudea, kila mumoja kwa kadiri alivyoweza kutoa.


Ingekuwa nimechagua kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe, ningeweza kungojea kupokea mushahara. Lakini kwa kuwa ni muzigo niliopewa, inanipasa kuitimiza.


Halafu watu wakafurahi kwa sababu walitoa kwa mapenzi yao, maana kwa moyo wao wote walimutolea Yawe kwa mapenzi yao, naye mufalme Daudi akafurahi sana.


Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.


Yule anayehubiri, anapaswa kutoa ujumbe wa Mungu. Na yule anayetumika, atumike kwa kadiri ya nguvu alizopewa na Mungu, kusudi Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa njia ya Yesu Kristo anayekuwa mwenye utukufu na uwezo kwa milele na milele. Amina.


Sisi tunawapenda sana hata tumekuwa tayari, si kuwatolea Habari Njema ya Mungu tu, lakini kutoa maisha yetu kwa ajili yenu vilevile. Ni vile kwa sababu ninyi mumekuwa kweli wapendwa wetu.


Ninaweza kushuhudia juu yake kwamba anajisumbua sana kwa ajili yenu na kwa ajili ya wandugu wa Laodikia na wa Hierapoli.


kwa maana Mungu anafanya kazi ndani yenu na kuwapa moyo wa kutaka na kutimiza mambo yanayolingana na mupango wake mwema.


Kwa maana ninashuhudia kwamba wanajitoa kwa bidii kutumikia Mungu, lakini bidii ile haitokani na ufahamu wa kweli.


Watu wako watajitolea, siku utakapokwenda kuwapiga waadui. Juu ya milima mitakatifu vijana wako watakufikia, kama umande unaotokeza asubui mapema.


Ninyi mulikuwa wenye furaha. Sasa nini imewatokea? Kwa maana ninaweza kuwashuhudia kwamba mungeweza kuongoa hata macho yenu na kuyatoa kwangu!


Amefanya sawa alivyoweza. Ameupakaa mwili wangu marasi mbele ya wakati kwa kuutayarisha kwa ajili ya maziko.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite