Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Wakorinto 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Sisi tunagandamizwa kila namna, lakini hatushindwi; tunahangaishwa, lakini hatukati tumaini;

Gade chapit la Kopi




2 Wakorinto 4:8
26 Referans Kwoze  

Kwa sababu hii ninafurahia uzaifu, matusi, ukosefu, taabu na mateso kwa ajili ya Kristo. Kwa maana wakati ninapokuwa muzaifu, basi ndio wakati ule ninapokuwa na nguvu.


Kwa maana hata wakati tulipofika Makedonia, hatukuweza kupumzika hata kidogo. Tulipata taabu pande zote: magomvi pamoja na watu wengine, na woga katika moyo wetu.


lakini Yawe hatamutoa mutu wa haki katika makucha yake, wala kumwachilia aazibiwe anaposhitakiwa.


“Sitawaacha kama wayatima, nitawarudilia tena.


Majaribu yale munayopata, ni yale yanayowapata watu wengine wote. Mungu hatawaachilia kujaribiwa kupita nguvu zenu, kwa maana yeye ni mwaminifu. Jaribu litakapowatokea, atawapatia nguvu ya kulivumilia, hata muweze kulishinda.


Lakini tunaonyesha katika mambo yote kwamba sisi ni watumishi wa Mungu: tumedumu sana katika mateso, katika ukosefu na katika taabu.


Anayemwogopa Yawe ana tumaini imara, na watoto wake watapata kimbilio salama.


Samweli akamwambia Saulo: “Kwa nini unanisumbua kwa kunipandisha?” Saulo akamujibu: “Mimi nina taabu kubwa! Wafilistini wananishambulia kwa vita, na Mungu ameniachilia. Hanijibu tena kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Ndiyo maana nimekuita unijulishe kitu cha kufanya.”


Sasa, Daudi alikuwa katika matatizo makubwa kwa sababu watu wake walikuwa na uchungu katika roho zao kwa kupoteza watoto wao. Kwa hiyo wakakuwa wakitaka kumupiga mawe. Lakini Daudi alijipa moyo kwa kumutegemea Yawe, Mungu wake.


Jina la Yawe ni munara imara; mwenye haki anaukimbilia na kuwa salama.


Halafu Saulo akamwambia mutu aliyemubebea silaha: “Chomoa upanga wako unichome nikufe, kusudi watu hawa wapagani wasikuje kunichoma upanga na kunichekelea.” Lakini yule aliyemubebea silaha hakusubutu kwa sababu aliogopa sana. Kwa hiyo, Saulo alitwaa upanga wake mwenyewe, na kuuangukia.


Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu, lakini hawakunishinda.


Lakini wote wanaomutumainia Yawe, watapata nguvu mupya. Watapanda juu kwa mabawa kama tai, watakimbia bila kuchoka, watatembea bila kuregea.


Hata kama miti ya tini isipochanua maua wala mizabibu kuzaa zabibu, hata kama mizeituni isipozaa zeituni na mashamba yasipotoa chakula, hata kama kondoo wakitoweka katika zizi na nyama wa kufugwa kukosekana katika mazizi,


Sisi hatukuwafungia mioyo yetu, lakini ni ninyi ndio muliotufungia moyo wenu.


Ningependa kuwa pamoja nanyi sasa, kwa maana ningetumia usemi mwingine. Ninashikwa na wasiwasi kwa ajili yenu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite