Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Wakorinto 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Ikiwa utumishi unaowaletea watu hukumu ulikuwa na utukufu, basi si zaidi sana utumishi unaowafanya watu wahesabiwe haki mbele ya Mungu, utakuwa na utukufu mukubwa zaidi?

Gade chapit la Kopi




2 Wakorinto 3:9
23 Referans Kwoze  

Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.


na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.


Lakini wale wanaotegemea kutimiza yale yanayoamuriwa na Sheria, wamelaaniwa. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Alaaniwe mutu yeyote asiyedumu katika yote yanayoandikwa katika hiki kitabu cha Sheria na kuyatii.”


Uzuri wa jua ni mbalimbali na uzuri wa mwezi, nao uzuri wa nyota ni mbalimbali, kwa maana hata nyota zinapishana uzuri vilevile.


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


Nyuma ya pale alitahiriwa, na kutahiriwa kwake kulikuwa kitambulisho cha kuhakikisha ile haki Mungu aliyomuhesabia kwa njia ya imani yake. Hivi Abrahamu akakuwa baba wa watu wote wanaoamini, ijapokuwa hawatahiriwi, kusudi wao vilevile wahesabiwe haki.


Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.


Siku ya kuwakomboa inakaribia, haiko mbali tena; siku ya kuwaokoa ninyi haitachelewa. Nitauokoa Sayuni, nitaleta utukufu kwa Israeli.


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote asiyekubali maneno haya ya sheria na kuyatii’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


Basi si zaidi sana matokeo ya utumishi wa Roho yatakuwa yenye utukufu?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite