Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Wakorinto 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Basi, nilikusudia kutorudia tena kwenu nikiwa mwenye huzuni.

Gade chapit la Kopi




2 Wakorinto 2:1
13 Referans Kwoze  

Ninamutaja Mungu kuwa mushuhuda wangu, yeye anajua roho yangu! Mimi nilikusudia kutorudia tena Korinto kwa sababu ya kuwasikilia huruma.


Ni kwa hiyo ninawaandikia maneno haya nikiwa mbali nanyi, kusudi wakati nitakapokuwa kati yenu nisitende kwa ukali kadiri ya mamlaka Bwana aliyonipa. Kwa maana uwezo ule ni kwa ajili ya kuwajenga katika imani, lakini si wa kubomoa.


Niliwaandikia nikiwa mwenye kusikitika sana na mwenye kufazaika kabisa na nikilia machozi mengi, si kwa kuwahuzunisha ninyi, lakini ni kusudi mupate kujua namna gani ninavyowapenda.


Basi munataka nini? Nifike kule kwenu, nikikuja na fimbo au na moyo unaojaa upendo na upole?


Wakati nitakapokutumia Artema au Tikiko, ufanye bidii sana kuja kukutana nami kule Nikopoli, kwa maana nimekusudia kukaa kule wakati wa baridi kali.


Ijapokuwa mimi ni mbali nanyi kimwili, mimi ni pamoja nanyi kiroho. Kwa hiyo nimefanya kama ningekuwa katikati yenu, maana yake, nimekwisha kumuhukumu kwa jina la Bwana wetu Yesu, yule mutu aliyetenda ubaya ule. Wakati mutakapokusanyika, mimi vilevile nitakuwa pamoja nanyi kiroho, nao uwezo wa Bwana Yesu utakuwa katikati yenu.


Kwa maana wakati nilipokuwa pamoja nanyi nilikusudia nisijue mambo mengine lakini Yesu Kristo tu na habari ya kufa kwake juu ya musalaba.


Basi Paulo na Barnaba wakapingana na kubishana nao vikali sana juu ya jambo hili. Na kwa hiyo wandugu waamini wakaagiza Paulo na Barnaba pamoja na watu wengine kati yao waende Yerusalema kusemezana na mitume na wazee wa kanisa la kule juu ya maneno yale.


Wanafunzi wakakusudia kutuma musaada kwa wandugu waamini waliokaa katika jimbo la Yudea, kila mumoja kwa kadiri alivyoweza kutoa.


Barnaba alitaka waende pamoja na Yoane, aliyeitwa vilevile Marko.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite