Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Wakorinto 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ingekuwa heri muvumilie kidogo masemi yangu ya upumbafu! Ninawaomba kweli munivumilie!

Gade chapit la Kopi




2 Wakorinto 11:1
17 Referans Kwoze  

Hii inatokana na kuona jinsi munavyomukubali mutu yeyote anayekuja kwenu na kuwahubiri habari za Yesu mwingine asiyekuwa yule sisi tuliyemuhubiri. Na zaidi ya hii munakubali upesi kupokea roho ingine na ujumbe mwingine vinavyokuwa tofauti na Roho au Habari Njema muliyopokea toka kwetu.


Mungu alikusudia kuwaokoa wale wanaomwamini kwa njia ya mahubiri tunayotangaza yanayoonekana kuwa mambo ya upumbafu. Amefanya vile kwa sababu, kwa njia ya hekima yao ya kimutu, watu hawakumutambua Mungu na hekima yake ya kimungu.


Ninasikia haya ya kuisema: tumekuwa zaifu kwa kufanya vile! Lakini kama watu wengine wanasubutu kujivuna juu ya kitu chochote, mimi vilevile nitajivuna. Sasa ninasema kama vile mupumbafu.


Ninyi munajidai kuwa wenye hekima na ndiyo maana munapenda kuwavumilia wapumbafu!


Ikiwa kweli tunaonekana kuwa wenda-wazimu, ni kwa ajili ya Mungu, lakini kama sisi ni wenye akili sawa, ni kwa faida yenu.


Kwa kuwa yeye mwenyewe ni muzaifu, anaweza kuwavumilia wale waliopotoka bila kujua.


Ninasema kama mupumbafu, lakini ni ninyi ndio mumenilazimisha kufanya vile. Kufuatana na ile, ningepaswa kusifiwa nanyi. Kwa maana hata kama mimi si kitu, wale mitume wenu wanaohesabiwa kuwa wakubwa hawanipiti kitu kabisa.


Sisi ni wapumbafu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika kuungana kwenu na Kristo. Sisi ni zaifu, lakini ninyi ni wenye nguvu. Tunazarauliwa, lakini ninyi munaheshimiwa!


Sasa mumekwisha kupata vyote munavyohitaji! Mumekwisha kuwa watajiri! Munakuwa wafalme ingawa sisi hatuko wafalme. Heri mungekuwa kweli watawala kusudi nasi vilevile tupate kutawala pamoja nanyi.


Mutu yeyote asijidanganye mwenyewe. Kama mutu fulani kati yenu akijizania kuwa mwenye hekima ya kidunia, ajifanye kama mupumbafu kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.


Paulo akajibu: “Ikiwa wakati kidogo au wakati murefu, ninamwomba Mungu, si juu yako wewe mwenyewe tu, lakini hata hawa wote wanaonisikiliza leo wapate kuwa sawa mimi, lakini wasifikie tu kutiwa katika kifungo!”


Paulo alipotaka kusema, Galio akawaambia Wayuda: “Kama mungemushitaki mutu huyu juu ya neno la uovu au kosa kubwa alilofanya, ningewasikiliza ninyi Wayuda vema.


Na Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka. Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Siku moja akamwambia bibi yake, muke wa Namani: “Ingekuwa heri bwana wangu angekwenda na kumwona yule nabii anayekuwa Samaria! Angemuponyesha ugonjwa wake.”


Yoshua akasema: “Ole wetu, ee Bwana wetu Yawe! Kwa nini umetuvukisha muto Yordani kwa kututia katika mikono ya Waamori kusudi watuangamize? Tungalifurahi kubaki ngambo ya muto Yordani!


Lakini Musa akamujibu: Unaona wivu kwa ajili yangu? Heri Yawe angewapa watu wake wote roho yake nao wapate kuwa manabii!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite