Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Wakorinto 10:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Sasa mimi Paulo mwenyewe ninawaomba kwa upole na kwa wema sawa na ule wa Kristo; mimi yule ambaye wanasema juu yake kwamba ni mupole wakati ninapokuwa pamoja nanyi, lakini ni mukali wakati ninapokuwa mbali nanyi.

Gade chapit la Kopi




2 Wakorinto 10:1
38 Referans Kwoze  

Kwa sababu wengi wanasema: “Barua za Paulo ni kali na zenye maneno mazito; lakini yeye mwenyewe anapokuwa katikati yetu ni muzaifu na namna yake ya kusema ni ya kuzarauliwa.”


Mukubali kuongozwa nami kama vile ngombe dume anayefungiwa nira, nanyi mufuate mafundisho yangu maana mimi ni mupole na munyenyekevu. Kwa hiyo mutapumzika.


Musikilize! Mimi Paulo ninataka kuwaambia kwamba kama mukikubali kutahiriwa, Kristo hana mafaa yoyote kwenu.


Basi wandugu zangu, kufuatana na vile Mungu alivyoonyesha huruma yake kwetu, ninawasihi mujitoe wenyewe kwake kuwa sadaka yenye uzima, takatifu na yenye kumupendeza. Hii ndiyo njia ya kweli ya kumwabudu.


Kama ikinipasa kujivuna nitajivuna kwa ajili ya uzaifu wangu.


Sababu ya hii nilikuwa kwenu katika hali ya uzaifu na woga, mwenye kutetemeka sana.


Mimi ni ndugu yenu Yoane. Kwa njia ya kuungana na Yesu, ninashirikiana nanyi katika mateso, katika ufalme wake na katika kuvumilia. Mimi nilikuwa nimepelekwa katika kisanga kinachoitwa Patimo, kwa sababu nilihubiri Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu.


Wapendwa wangu, ninawasihi ninyi, kama vile wageni na wasafiri hapa katika dunia, muepuke tamaa za mwili zinazopigana na roho.


lakini kwa ajili ya upendo, ninapendelea kukusihi, mimi Paulo ninayekuwa muzee, na zaidi sasa ninakuwa mufungwa kwa ajili ya Yesu Kristo.


Hii ni salamu ninayoiandika kwa mukono wangu mimi Paulo mwenyewe. Hii ndiyo sahihi yangu katika kila barua yangu, na mwandiko wangu.


Kwa hivi basi, mimi ninayekuwa mufungwa kwa sababu ninamutumikia Bwana, ninawasihi muishi sawa inavyostahili kufuatana na mwito Mungu aliowatolea.


Munakumbuka kwamba niliwahubiri Habari Njema kwa mara ya kwanza kwa sababu ya ugonjwa nilioupata.


Basi, nitajivuna kwa ajili ya mutu sawa na yule, lakini sitajivuna kwa ajili yangu mimi mwenyewe, isipokuwa tu kwa ajili ya uzaifu wangu.


Ninasikia haya ya kuisema: tumekuwa zaifu kwa kufanya vile! Lakini kama watu wengine wanasubutu kujivuna juu ya kitu chochote, mimi vilevile nitajivuna. Sasa ninasema kama vile mupumbafu.


Ninyi munaangalia tu namna vitu vinavyoonekana kwa inje. Mutu yeyote anayejiaminia kwamba yeye ni wa Kristo, inafaa afikiri tena yeye mwenyewe mambo haya: ikiwa yeye ni wa Kristo sisi vilevile ni wa Kristo.


Ninawasihi kwamba nitakapofika kwenu, musinisukume kuwa mukali. Kwa maana nina uhakika kwamba nitawatendea vile wale watu wote wanaozania kwamba sisi tunaishi maisha ya kimwili.


Mimi ninawaaminia sana na kujivuna kwa ajili yenu. Katika mateso yetu yote, ninafarijiwa sana na kujazwa na furaha.


Basi, sisi tunaotumika pamoja na Mungu, tunawasihi musipoteze bure neema muliyopokea kwake.


Basi sisi ni wajumbe wa Kristo. Kwa njia yetu, Mungu mwenyewe anawaita ninyi; na kwa hiyo tunawasihi katika jina la Kristo, mukubali kupatanishwa na Mungu.


Na kwa sababu tunakuwa na tumaini lile, sisi tunasema kwa uhodari.


Sisi ni wapumbafu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika kuungana kwenu na Kristo. Sisi ni zaifu, lakini ninyi ni wenye nguvu. Tunazarauliwa, lakini ninyi munaheshimiwa!


Lakini mara moja moja nimewaandikia kwa uhodari juu ya mambo fulani kusudi niwakumbushe tena mambo yale. Nimefanya vile kutokana na neema ile niliyopewa na Mungu


Isaya kwa uhodari anaongeza kusema maneno haya: “Nimepatikana kwa watu wasionitafuta, nimejifunua kwa watu wasioniuliza.”


Na sehemu ya Maandiko aliyokuwa akisoma ni hii: “Alipelekwa kama kondoo kwenda kuchinjwa, kama mwana-kondoo anayenyamaza mbele ya mwenye kumukata manyoya. Yeye hakufungua kinywa chake.


“Muwaambie wakaaji wa muji Sayuni: ‘Angalia, mufalme wenu anakuja kwenu. Yeye ni munyenyekevu, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, kitoto cha punda.’ ”


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Ujifungie upanga wako, ewe shujaa! Wewe ni mutukufu na mwenye mamlaka.


Basi munataka nini? Nifike kule kwenu, nikikuja na fimbo au na moyo unaojaa upendo na upole?


Kufuatana na mambo hayo, mimi Paulo, mufungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu ninyi watu wa mataifa mengine, ninamwomba Mungu.


Muonyeshe upole wenu kwa watu wote, kwa maana Bwana yuko karibu kurudia.


Lakini, inawapasa ninyi kuendelea na musingi imara katika imani, musitikiswe na kupoteza lile tumaini mulilopata wakati muliposikia Habari Njema. Mimi Paulo nimewekwa kuwa mutumishi wa kuhubiri Habari Njema ile iliyokwisha kutangazwa kwa watu wote katika dunia.


Mimi Paulo ninaandika kwa mukono wangu mwenyewe maneno haya: nitakulipa. (Sitaki kusema kwamba maisha yako ni deni unalokuwa nalo kwangu.)


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite