Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Wafalme 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mumwambie mufalme kwamba Yawe amesema hivi: ‘Hautashuka katika kitanda ulichopanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”

Gade chapit la Kopi




2 Wafalme 1:4
14 Referans Kwoze  

Mujue kwamba uzima wa kila mutu ni katika mikono yangu, ikiwa uzima wa muzazi na uzima wa mutoto. Yeyote anayetenda zambi, ndiye atakayekufa.


Nyoka akamwambia mwanamuke: “Hamutakufa!


Lakini usikule matunda ya muti wa kujua mazuri na mabaya, maana siku utakapokula matunda ya muti ule, hakika utakufa.”


Mutu anayekusudia kuwa mwenye haki ataishi, lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.


Akamwambia mufalme: “Yawe anasema hivi: ‘Kwa sababu ulituma wajumbe kuomba shauri kwa Bali-Zabubu mungu wa Ekuroni sawa vile hakuna Mungu katika Israeli ambaye ungemwomba shauri, basi, hautashuka katika kitanda ambacho umepanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”


Zaidi ya hayo, Yawe atakutia wewe pamoja na Waisraeli wote katika mikono ya Wafilistini. Kesho, wewe na wana wako mutakuwa pamoja nami. Hata waaskari wa Israeli, Yawe atawatia katika mikono ya Wafilistini.”


Mwovu anaangamizwa kwa matendo yake maovu, lakini mwenye haki atapata usalama kwa uaminifu wake.


Wakamujibu: “Tumekutana na mutu ambaye alitutuma turudi kukuambia kwamba Yawe amesema hivi: ‘Kwa nini unatuma wajumbe kwa Bali-Zebubu, mungu wa Ekuroni? Hakuna Mungu katika inchi ya Israeli? Hautashuka katika kitanda ulichopanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”


Ahiya akamwambia muke wa Yeroboamu: “Simama, urudie kwako sasa. Mara tu utakapoingia katika muji, mwana wako atakufa.


Yawe alikuwa amesema kwamba wote watakufia katika jangwa, na kweli hakuna hata mumoja wao aliyebaki muzima, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.


Basi, Elia akawaendea. Wale wajumbe wakarudi kwa mufalme, naye akawauliza: “Mbona mumerudia?”


Basi, Elia akaenda kujionyesha kwa Ahabu. Wakati huo, njaa ilikuwa kali sana kule Samaria.


Basi Elisha akamujibu: “Umwambie kwamba atapona. Lakini Yawe amenionyesha kwamba atakufa.”


Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya, mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: “Yawe amesema hivi: ‘Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.’ ”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite