Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 8:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Daudi aliteka waaskari wapanda-farasi elfu moja na mia saba, na waaskari wa miguu elfu makumi mbili. Kisha Daudi alikata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wa magari ya vita, lakini aliacha farasi wa kutoshelea kwa magari mia moja.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 8:4
8 Referans Kwoze  

Yoshua akakatakata mishipa ya miguu ya farasi wao wote na kuyateketeza magari yao kwa moto, kama Yawe alivyomwagiza.


Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hao, maana kesho, wakati kama huu, nitawaangamiza wote kwa kuwatia katika mikono ya Waisraeli; nanyi mutakata mishipa ya miguu ya farasi wao na kuteketeza magari yao kwa moto.”


Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua, atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni; kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa.


Daudi akanyanganya magari ya vita elfu moja, waaskari wapanda-farasi elfu saba na wa miguu elfu makumi mbili. Kisha Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wa magari, lakini akaacha mia moja.


Solomono alikusanya magari ya vita na waaskari wapanda-farasi. Alikuwa na magari ya vita elfu moja na mia ine na waaskari wapanda-farasi elfu kumi na mbili ambao aliwaweka katika miji yenye vituo vya magari ya vita, na kule Yerusalema.


Hata hivyo, asikuwe na farasi wengi kwa ajili yake mwenyewe, wala asiwarudishe watu Misri kwa kujipatia farasi zaidi, kwa sababu Yawe amewaonya: ‘Hamutarudi tena kwa njia ile.’


lakini mimi sitashiriki mashauri yao mabaya. Ee roho yangu, usishiriki mikutano yao, maana, katika hasira yao, walimwua mutu, kwa mapenzi yao walikata mushipa wa ngombe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite