Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 8:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Akaweka kambi za waaskari katika inchi ya Edomu yote. Nao Waedomu wote wa kule wakakuwa watumishi wake. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 8:14
18 Referans Kwoze  

Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”


Halafu Daudi aliweka kambi za waaskari katika muji wa Waaramu wa Damasiki. Basi, Waaramu wakakuwa watumishi wake na wakakuwa wanamulipa kodi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Yawe akamwambia: “Mataifa mawili yako ndani ya tumbo lako; makabila mawili yatakayozaliwa nawe, yatatengana. Moja litakuwa lenye nguvu kuliko lingine, mukubwa atamutumikia mudogo.”


Basi akaweka kambi za waaskari kule Edomu. Nao Waedomu wote wakakuwa watumishi wa Daudi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Waasherati wote wa kidini waliobaki tangu nyakati za baba yake Asa, Yosafati aliwaondoa katika inchi.


Kwa hiyo, Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akawahukumu watu wake wote kufuatana na haki na sheria.


Wakati Daudi alipowaangamiza Waedomu, Yoabu, jemadari wa waaskari wa Daudi, alikwenda kule kuwazika waliouawa. Yoabu aliwaua wanaume wote wa Edomu.


Naye Daudi akazidi kuwa na uwezo zaidi kwa sababu Yawe, Mungu wa majeshi, alikuwa pamoja naye.


Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye utukufu kama wakubwa wengine katika dunia.


Katika inchi ya Edomu, hakukuwa mufalme. Inchi hiyo ilitawaliwa na musimamizi.


Amazia aliwaua Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi. Aliutwaa kwa nguvu muji wa Sela na kuuita Yokiteli, na hivi ndivyo unavyoitwa mpaka sasa.


Basi, Yawe alikuwa pamoja naye, na alimwezesha kwa kila jambo alilotenda. Alimwasi mufalme wa Asuria na kukataa kumutumikia.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo “Ushuhuda wa mayungiyungi.” Mashairi ya Daudi ya kufundisha yanayoelekea wakati alipopigana na Wasuria katika Mesopotamia na Zoba naye Yoabu aliporudi nyuma na kuwaua Waedomu elfu kumi na mbili katika bonde la Chumvi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite