Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 7:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Kutokana na yale tuliyosikia, wewe Yawe ni mukubwa. Hakuna anayekuwa kama wewe, na hakuna Mungu mwingine lakini wewe.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 7:22
33 Referans Kwoze  

Wewe ndiwe mukubwa, unafanya maajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.


Ee Bwana, hakuna mungu mwingine anayekuwa kama wewe; hakuna anayeweza kufanya unayofanya wewe.


“Ewe Yawe, ni nani kati ya miungu anayelingana nawe? Ni nani aliyekuwa kama wewe unayekuwa mutakatifu mukubwa, unayetisha kwa matendo matukufu, unayetenda mambo ya ajabu?


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Maana Yawe ni mukubwa, anasifika sana anastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.


Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine; hakuna Mungu mwingine lakini mimi. Ninakuimarisha ingawa wewe haunijui,


‘Ee Bwana wetu Yawe, ninajua umenionyesha mimi mutumishi wako mwanzo tu wa ukubwa wako na uwezo wako. Maana, kuna mungu gani huko mbinguni au katika dunia anayeweza kufanya mambo makubwa na ya ajabu kama vile ulivyofanya wewe?


Hakuna anayekuwa mutakatifu kama Yawe; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye; hakuna anayekuwa jiwe la kufichamia kama Mungu wetu.


Wewe unatisha katika baraza la watakatifu; wote wanaokusanyika mbele yako wanakuheshimu na kukuogopa.


Ee Yawe, mbingu zinasifia maajabu yako, uaminifu wako unasifiwa katika kusanyiko la watakatifu.


Maana Yawe ni mukubwa, anasifiwa sana; anastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.


Ninyi mulijaliwa kuona mambo hayo, kusudi mupate kutambua kwamba Yawe ndiye peke yake Mungu na wala hakuna mwingine.


Mutamulinganisha Mungu na nini basi, au ni kitu gani cha kumufananisha nacho?


Yawe ni mukubwa, anastahili sifa nyingi; ukubwa wake hauwezi kuchunguzika.


Ninajua hakika kwamba Yawe ni mukubwa; Bwana wetu ni mukubwa kupita miungu yote.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Mashairi ya Wakora.


Basi, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninachotaka kufanya si kwa faida yenu ninyi watu wa inchi ya Israeli, lakini ni kwa heshima ya jina langu takatifu mulilolikufuru kati ya mataifa mulikokwenda.


Munigeukie mimi mupate kuokolewa, popote munapokuwa katika dunia. Maana mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.


Mungu Mutakatifu anauliza hivi: Basi, mutanilinganisha na nani? Kuna mutu anayeweza kuwa sawasawa mimi?


Lakini ni nani anayeweza kumujengea nyumba ikiwa mbingu zenyewe hazimutoshi, wala mbingu za juu sana? Nami ni nani basi, hata nimujengee nyumba isipokuwa tu kama pahali pa kufukizia ubani mbele yake?


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Lakini mujue kwamba sitafanya hivyo kwa ajili yenu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Lakini mupate haya na kufazaika kwa sababu ya matendo yenu, enyi Waisraeli!


na ninyi mupate kuwaelezea watoto wenu na wajukuu wenu jinsi nilivyowachekelea Wamisri kwa kuonyesha vitambulisho vile kati yao. Hivyo mutatambua kwamba mimi ni Yawe.”


Watu wakawakusanya vyura wale malundomalundo. Inchi nzima ikanuka.


Maana mara hii, wewe mwenyewe, wakubwa wako na watu wako mutapatwa na mapigo yangu makali. Nawe utatambua kwamba hakuna yeyote katika dunia anayekuwa kama mimi.


akasema: “Ee Yawe, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu mwingine kama wewe, juu mbinguni, au chini katika dunia. Wewe unashika agano lako na kutenda wema kwa watumishi wako wanaoishi wakikutii kwa moyo wao wote.


Uliliona jiwe lililoongoka lenyewe toka kwenye mulima, bila kuguswa, na jinsi lilivyoivunja vipandevipande ile sanamu iliyotengenezwa kwa chuma, shaba, udongo wa mufinyanzi, feza na zahabu. Ee mufalme, Mungu Mukubwa amekufunulia mambo yatakayotukia nyuma. Ni mimi ninayekuelezea hivyo. Ndoto yako ni ya kweli na maana yake ni ya kuaminiwa.


Mufalme wa Misri akamwambia: “Kesho.” Musa akasema: “Nitafanya kama vile unavyosema, kusudi ujue kwamba hakuna yeyote anayelingana na Yawe, Mungu wetu.


Basi, mukumbuke leo na kuweka ndani ya mioyo yenu, kwamba Yawe ndiye Mungu juu mbinguni na chini katika dunia. Hakuna mwingine.


Nani anayekuwa Mungu isipokuwa Yawe? Nani anayekuwa kikingio isipokuwa Mungu wetu?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite