Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 mufalme Daudi akamwambia nabii Natani: “Angalia, mimi ninakaa katika nyumba iliyojengwa na miti ya mierezi, lakini Sanduku la Mungu linakaa ndani ya hema.”

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 7:2
24 Referans Kwoze  

Kisha, mufalme Hiramu wa Tiro alituma wajumbe kwa Daudi. Alimupelekea vilevile miti ya mierezi, waseremala na wajengaji ambao walimujengea Daudi nyumba ya kifalme.


Basi Yawe akamutuma nabii Natani kwa Daudi. Natani alimwendea Daudi, akamwambia: “Kulikuwa wanaume wawili katika muji mumoja. Mumoja alikuwa tajiri na mwingine alikuwa masikini.


Mungu akamujalia Daudi neema hata akamwomba yeye Mungu wa Yakobo ruhusa ya kumujengea nyumba.


Wanafunzi wake wakakumbuka maneno haya yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Upendo wangu kwa ajili ya nyumba yako unanichoma.”


Ni sawa kwenu kukaa katika nyumba zenu nzuri wakati nyumba yangu ni mabomoko matupu?


Habari za mufalme Daudi toka mwanzo mpaka mwisho juu ya mambo ya utawala wake, uwezo wake, na mambo yaliyomupata yeye, Waisraeli, na falme zote katika inchi zimeandikwa katika vitabu vya nabii Samweli, katika vitabu vya nabii Natani, vilevile katika vitabu vya nabii Gadi.


Kisha wakaingiza Sanduku la Agano, na kuliweka ndani ya hema ambayo Daudi alikuwa ametayarisha. Halafu wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto na za amani mbele ya Mungu.


mpaka nikutayarishie wewe Yawe nafasi ya kukaa, ndiyo makao yako, ewe Mwenye Nguvu wa Yakobo!”


(Lakini, sanduku la Mungu lilikuwa Yerusalema katika hema ambalo mufalme Daudi alilipigia alipolileta kutoka Kiriati-Yearimu).


Kisha mufalme Hiramu wa Tiro akatuma wajumbe kwa Daudi, akamupelekea vilevile miti ya mierezi, wajengaji na waseremala, kusudi wamujengee Daudi nyumba ya kifalme.


Natani alimwelezea Daudi kila kitu ambacho alionyeshwa katika maono hayo na Mungu.


Kisha waliliingiza Sanduku la Yawe ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha pale na kuliweka pahali pake. Naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele ya Yawe.


Kisha akaweka lile Sanduku la Agano ndani ya hema na kutundika pazia, na kwa namna hiyo akafunika Sanduku la Agano, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Uria alimujibu Daudi: “Sanduku la Agano, pamoja na waaskari wote wa Israeli na Yuda wanakaa kwenye vibanda katika vita. Bwana wangu Yoabu na watumishi wake wote wamepiga kambi katika mbuga. Basi ni vizuri mimi niende nikule na kunywa na kulala na muke wangu? Ninaapa kwamba, kama vile unavyoishi, sitafanya kitu cha namna ile.”


Wakati Batiseba alipokuwa akizungumuza na mufalme, nabii Natani aliingia katika nyumba ya kifalme.


Kwa hiyo, baba yangu alikusudia kumujengea Yawe, Mungu wa Israeli nyumba.


Daudi akamwambia Solomono: “Mwana wangu, nilikusudia ndani ya moyo wangu kumujengea Yawe, Mungu wangu, nyumba kwa kumutukuza.


Matendo mengine ya Solomono, kutoka mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika kitabu cha “Historia ya Nabii Natani,” katika “Unabii wa Ahiya wa Shilo,” na katika “Maono ya Ido Mwonaji,” juu ya Yeroboamu mwana wa Nebati.


Mufalme Hezekia alifuata maagizo ambayo Yawe alikuwa amemupa mufalme Daudi kwa njia ya Gadi, nabii wa mufalme na nabii Natani. Hivyo basi, akaweka Walawi katika nyumba ya Yawe, wamoja wao wakiwa na matoazi, wengine vinanda na wengine vinubi. Hiyo ilikuwa amri ya Yawe kwa njia ya manabii wake.


Lakini kuhani Zadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, nabii Natani na Simei, na Rei pamoja na walinzi wa Daudi, hawakumwunga Adonia mukono.


Ukumbuke ahadi aliyokupa, ee Yawe, ndicho kiapo alichokuapia, ewe Mwenye Nguvu wa Yakobo. Alisema:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite