Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 7:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwana wangu. Akifanya maovu, nitamwazibu kama vile wanadamu wanavyowaazibu watoto wao kwa fimbo.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 7:14
19 Referans Kwoze  

Kwa maana Mungu hakumwambia hata mara moja mumoja wa wamalaika wake hivi: “Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.” Wala hakusema maneno haya juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwana wangu.”


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


“Yawe aliniambia: ‘Mwana wako Solomono ndiye atakayenijengea nyumba na viwanja vyangu, kwa maana nimemuchagua yeye akuwe mwana wangu, nami nitakuwa baba yake.’


Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwana wangu. Sitaacha kumutendea mema kama vile nilivyoacha kumutendea Saulo aliyekutangulia.


Mukumbuke kwamba Yawe, Mungu wenu, anawaazibu kama vile baba anavyoazibu mwana wake.


Lakini tunahukumiwa na kuazibiwa na Bwana kusudi tusiazibiwe pamoja na watu wa dunia hii.


Maana mimi niko pamoja nawe, nipate kukuokoa. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote, ambayo niliyokusambaza kati yao; lakini sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakuazibu kadiri unavyostahili wala sitakuachilia uende bila kukuazibu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Heri mutu yule anayeazibiwa na Mungu! Hivyo usizarau Mungu Mwenye Uwezo anapokuazibu.


Nitakuwa Baba yenu nanyi mutakuwa wana na wabinti wangu. Ni mimi Bwana Mwenye Uwezo ninayesema.”


Yule atakayeshinda atapokea toka kwangu zawadi ile, mimi nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwana wangu.


Lakini wewe au watoto wako mukigeuka na kuacha kunifuata, musiposhika amri zangu na masharti niliyowapa, mukienda kutumikia miungu mingine na kuiabudu,


Hata hivyo, sitamunyanganya urizi wote, wala sitamwondolea mamlaka wakati angali anaishi, kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi ambaye nilimuchagua, na ambaye alifuata amri zangu na masharti yangu.


Hivyo, yeye ndiye atakayenijengea nyumba. Atakuwa mwana wangu nami nitakuwa baba yake, na wazao wake watatawala Israeli milele.’


Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite