Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 7:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu na kiti chake cha kifalme cha ufalme wake nitakiimarisha milele.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 7:13
39 Referans Kwoze  

Hata hivyo, si wewe utakayenijengea nyumba, lakini ni mwana wako utakayemuzaa ndiye atakayenijengea hiyo nyumba.’


Siku zote za utawala wake, watu wa Yuda na wa Israeli walikaa salama, kila mutu akistawi kwenye miti yake ya mizabibu na ya tini.


Wewe umesema: “Nimefanya agano na muchaguliwa wangu, nimemwapia mutumishi wangu Daudi hivi:


“Juu ya nyumba hii unayoijenga, kama ukifuata masharti yangu, ukiyatii maagizo yangu na amri zangu zote, nitakutimizia mambo yote niliyomwahidi baba yako Daudi.


Yeye ndiye atakayelijenga hekalu la Yawe. Atapewa heshima ya kifalme na kuikaa kwenye kiti chake cha kifalme kuwatawala watu wake. Kuhani Mukubwa ataikaa karibu na kiti cha kifalme cha mutawala yule, nao wawili watafanya kazi pamoja kwa amani.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Nitamwonyesha wema wangu kwa milele, na agano langu kwake litadumu siku zote.


Ukoo wako na ufalme wako vitadumu imara siku zote. Kiti chako cha kifalme kitakuwa imara milele.”


Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.


Mujengaji wa nyumba anaheshimiwa zaidi kuliko nyumba yenyewe. Hivi vilevile Yesu anastahili kupewa heshima kubwa zaidi kuliko Musa.


Yawe anasema hivi: Wakati uliofaa nilijibu maombi yako; wakati wa wokovu nilikusaidia. Nimekuweka na kukufanya ukuwe kiungo cha agano langu na mataifa yote: utatengeneza inchi na kurudisha tena inchi hiyo iliyoharibika.


Nimemupata mutumishi wangu Daudi; nimemuchagua kwa kumupakaa mafuta yangu matakatifu.


Basi fanya angalisho na kukumbuka kwamba Yawe amekuchagua wewe umujengee nyumba ya ibada. Ukuwe hodari na utende hivyo.”


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Maana wewe, ee Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, umenifunulia mimi mutumishi wako, ukisema: ‘Nitakujengea nyumba’; ndiyo maana nina uhodari wa kutoa ombi hili mbele yako.


Naye Yawe atatimiza ahadi yake aliyotoa aliponiambia kwamba, ikiwa wazao wangu watatii amri zake na kumutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wote, hakutakosekana mumoja wao kwa kutawala Israeli nyakati zote.


Sasa basi, kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyeniweka na kuniimarisha katika ufalme wa baba yangu Daudi na kutimiza ahadi yake ya kunipa kiti cha kifalme mimi na wazao wangu, Adonia atakufa leo!”


Lakini mimi atanibariki, na kiti cha kifalme cha Daudi kitaimarishwa mbele ya Yawe milele.”


Hakika, nimekujengea nyumba ya kukaa, pahali pa makao yako ya milele.”


akasema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, maana kwa nguvu yake ametimiza ahadi yake aliyomupa baba yangu Daudi, akisema:


Alijenga mazabahu katika nyumba ya Yawe pahali ambapo Yawe alikuwa amesema: “Jina langu litaabudiwa katika Yerusalema.”


Alijenga tena mazabahu katika nyumba ya Yawe pahali ambapo Yawe alikuwa amesema: “Jina langu litaabudiwa milele katika Yerusalema.”


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Mungu anamujalia mufalme wake ushindi mukubwa; anamutendea mema muchaguliwa wake, ndiye Daudi na wazao wake milele.


Lakini Yawe hakutaka kuangamiza Yuda, kwa sababu ya Daudi mutumishi wake, maana aliahidi kwamba wazao wake wataendelea kutawala milele.


Nayo sanamu ya Ashera aliyotengeneza akaiweka katika nyumba ambayo Yawe alisema juu yake mbele ya Daudi na mwana wake Solomono: “Katika nyumba hii na katika Yerusalema niliouchagua ndipo pahali nitakapoabudiwa milele.


“Kwa hiyo sasa, Ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba tena utimize ile ahadi uliyomwahidi mutumishi wako Daudi baba yangu, ukisema: ‘Siku zote utakuwa na mutu wa uzao wako wa kuikaa katika kiti cha kifalme cha Israeli, ikiwa wazao wako wataangalia mwenendo na kushika sheria zangu kama vile wewe ulivyofanya mbele yangu.’


Haachi kuwalinda watu wa haki; nao anawaweka kuwa wafalme watawale na kutukuzwa.


Jina la mufalme litukuzwe siku zote; utukufu wake udumu muda wote jua litakapokuwa. Kwake mataifa yote yabarikiwe; watu wote wamwite mwenye heri!


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Maana Yawe anasema hivi: Hakutakosekana hata kidogo mutu wa uzao wa Daudi atakayetawala Waisraeli.


Watakaa katika inchi ya wazee wao ambayo nilimupa Yakobo. Wao na watoto wao na wajukuu wao wataishi humo milele. Naye Daudi, mutumishi wangu, atakuwa mutawala milele.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


na kumwambia kwamba Yawe wa majeshi anasema hivi: Hapa kuna mutu anayeitwa Tawi. Yeye atastawi pale anapokuwa na kulijenga hekalu la Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite