Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 7:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nami nitawachagulia watu wangu wa Israeli pahali pa kuishi niwapandikize kusudi waishi pahali pao wenyewe, wasisumbuliwe tena. Nao watu wakali hawatawatesa tena kama zamani,

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 7:10
25 Referans Kwoze  

Nitawasimika katika inchi yao, wala hawataongolewa tena kutoka katika inchi niliyowapa. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Nami nitawachagulia watu wangu wa Israeli pahali pa kuishi niwapandikize, kusudi waishi pahali pao wenyewe, wasisumbuliwe tena. Nao watu wakali wanaotumia nguvu hawatawatesa tena kama zamani,


Nitawalinda siku zote na kuwarudisha katika inchi hii. Nitawajenga, wala sitawabomoa; nitawapanda, wala sitawaongoa.


Mateso makali hayatasikilika tena katika inchi yako; wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako. Utaweza kuziita kuta zako: “Wokovu”, na milango yako: “Sifa”.


Mungu anasema: Mataifa jirani za Waisraeli ambayo yalikuwa yanawauzi hayataweza tena kuwaumiza Waisraeli kama vile kwa miiba na michongoma. Halafu watajua kwamba mimi ni Bwana wao Yawe.


Ee Mungu wa majeshi, utengeneze tena maisha yetu, utuangalie kwa wema, nasi tutaokoka.


Vilevile inaweza kunifikia kukusudia wakati wowote juu ya taifa au ufalme fulani kwamba nitalijenga na kulistawisha.


Yeye atapanguza machozi yao yote na kifo hakitakuwa tena, wala kilio, wala malalamiko, wala maumivu. Kwa maana dunia ya mbele imekwisha kupita.”


Siku hiyo, wewe utaniita “Mume wangu”, na sio tena “Bali wangu”. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Wewe utawaleta watu wako na kuwapanda juu ya mulima wako, pale ulipochagua, ee Yawe, kuwa makao yako, pahali patakatifu, ee Yawe, ulipojenga kwa mikono yako.


Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!


Alililima vizuri na kuondoa mawe yote, akapanda humo mizabibu bora, alijenga munara wa ulinzi katikati yake, akachimba kikamulio cha divai. Kisha akatazamia lizae zabibu nzuri. Lakini likazaa zabibu chungu.


Watu wako hawakuitwaa inchi kwa silaha zao, wala hawakupata ushindi kwa nguvu zao, lakini kwa mukono wako mwenyewe, kwa kuwaangazia uso wako, maana wewe uliwapenda.


Mufalme Asikie alikuwa na magari ya vita mia tisa ya chuma. Aliwagandamiza sana Waisraeli kwa miaka makumi mbili; nao wakamulilia Yawe awasaidie.


Wafilistini walitoka kwenye kambi yao kwenda kuwashambulia wakiwa katika vikundi vitatu. Kikundi kimoja kilielekea Ofura katika inchi ya Suali.


Kisha mufalme wa Misri akawaamuru watu wake wote hivi: “Kila mutoto mwanaume atakayezaliwa kwa Waebrania mumutupe ndani ya muto Nili. Lakini kila mutoto mwanamuke, mumwache aishi.”


Na ikiwa Waisraeli watajali kutenda yote niliyowaamuru na kufuata sheria zote mutumishi wangu Musa alizowapa, basi sitawaacha wafukuzwe kutoka katika inchi hii ambayo niliwapa babu zao.”


Na ikiwa watu wa Israeli watajali kutenda yote niliyowaamuru, Sheria yote, masharti, na maagizo yaliyotolewa kwa mukono wa Musa, basi sitawaacha hata kidogo wafukuzwe kutoka katika inchi hii ambayo niliwapa babu zao.”


Ee Mungu, sisi tumesikia kwa masikio yetu, babu zetu wametuelezea mambo uliyotenda nyakati zao, ndiyo mambo uliyotenda hapo kale.


Uliongoa muzabibu kutoka Misri; ukawafukuza watu wa mataifa, na kuupandikiza katika inchi yao.


Watu wako wote watakuwa wa haki, nao watarizi inchi milele. Hao ni chipukizi nililopanda mimi, kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite