Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Halafu walikamata kichwa cha Isiboseti na kumupelekea Daudi kule Hebroni. Nao wakamwambia mufalme Daudi: “Hiki ni kichwa cha Isiboseti mwana wa Saulo ambaye ni adui yako aliyekuwa anataka kuyaangamiza maisha yako. Yawe leo amekulipizia kisasi juu ya Saulo na wazao wake.”

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 4:8
18 Referans Kwoze  

Kukitokea watu wanaokufuatilia na kutaka kuyaangamiza maisha yako, Yawe, Mungu wako, atayalinda maisha yako pamoja na watu wanaokuwa wazima. Lakini atayatupilia mbali maisha ya waadui zako, kama vile mutu anavyotupa jiwe kwa mujeledi.


Yeye ameniwezesha kulipiza kisasi, ameweka mataifa chini yangu.


Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!


Watu wale wakalalamika hivi kwa sauti kubwa: “Bwana mutakatifu na mwenye ukweli, mpaka wakati gani utaendelea kungojea kuwahukumu wakaaji wa dunia na kuwaazibu kwa sababu ya kuuawa kwetu?”


Akamwambia: “Amuka, utwae mutoto pamoja na mama yake, na urudie nao katika inchi ya Israeli, kwa maana wale waliotafuta kumwua wamekwisha kufa.”


Nitatangaza haki yako muchana kutwa, maana wanaonitakia hasara wamefezeheka na kuzarauliwa.


Halafu yule Mwetiopia akafika; naye akasema: “Kuna habari njema kwako bwana wangu mufalme! Maana Yawe leo hii amekukomboa kutoka nguvu za wale wote waliokushambulia.”


Kisha, Ahimasi mwana wa Zadoki, akasema: “Uniruhusu nikimbie kumupelekea mufalme habari hizi kwamba Yawe amemukomboa toka katika nguvu za waadui zake.”


Saulo alipokuwa anasafiri, alifika kwenye pango moja lililokuwa karibu na zizi la kondoo, akaingia mule ndani ya pango kwa kujisaidia. Daudi na watu wake walikuwa wakiikaa ndani kabisa ya pango lile.


Daudi alijua kwamba Saulo alitaka kuyaangamiza maisha yake. Daudi akabaki katika mbuga za Zifu, kule Horeshi.


Daudi alikimbia kutoka Nayoti katika Rama, akaenda mpaka kwa Yonatani, akamwambia: “Nimefanya nini? Kosa langu ni gani? Nimemutendea baba yako zambi gani hata anajaribu kuyaangamiza maisha yangu?”


Kisha Saulo akawatuma warudie kule tena, akawaagiza akisema: “Mumulete Daudi kwangu hata akiwa katika kitanda kusudi auawe.”


Basi, alimutupia Daudi mukuki mara mbili maana alifikiri: “Nitamubanisha Daudi kwenye ukuta.” Lakini Daudi aliepa mara zote mbili.


Abeneri mwana wa Neri, mukubwa wa waaskari wa Saulo alikuwa amemukamata Isiboseti mwana wa Saulo na kumupeleka kule Mahanaimu.


Saulo alimwelezea mwana wake Yonatani na wakubwa wake juu ya mupango wake wa kumwua Daudi. Lakini Yonatani, mwana wa Saulo, alimupenda sana Daudi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite