Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Abeneri alikasirika sana kutokana na maneno ya Isiboseti, akasema: “Unafikiri mimi ni imbwa anayeitumikia jamaa ya Yuda? Angalia, mimi nimewatendea mema jamaa ya baba yako Saulo, wandugu zake, na warafiki zake na sikukutoa kwa Daudi mpaka leo. Hata hivyo, leo hii unaniona kuwa mwenye kosa kwa ajili ya mwanamuke.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 3:8
16 Referans Kwoze  

Mefiboseti akainama, na kusema: “Mimi ni sawa na imbwa mufu. Kwa nini unishugulikie hivyo?”


Kwa hiyo, Abisayi mwana wa Zeruya akamwambia mufalme: “Kwa nini huyu anayekuwa sawa imbwa mufu akulaani wewe bwana wangu mufalme? Uniruhusu nimwendee, nami nitakikata kichwa chake.”


Wewe umemutukana nani? Umemutusi nani? Umesubutu kumufokea nani kwa majivuno? Ni Mungu, Mutakatifu wa Israeli!


wakati ulipoinuka kutimiza hukumu, kuwaokoa wote wanaoteswa katika dunia.


Hazaeli akauliza: “Lakini mimi mutumishi wako ni kitu kweli? Mimi ninayekuwa sawa na imbwa nitaweza namna gani kutenda mambo hayo makubwa?” Elisha akamujibu: “Yawe amenionyesha kwamba utakuwa mufalme wa Aramu.”


Zamani, Saulo alipokuwa mufalme wetu wewe ndiwe uliyewaongoza Waisraeli katika vita, na Yawe alikuambia: ‘Utakuwa muchungaji wa watu wangu Waisraeli; utakuwa mukubwa juu ya inchi ya Israeli.’ ”


Sasa, mulilete jambo hilo mbele ya watu kwa sababu Yawe alimwahidi Daudi hivi: ‘Kwa mukono wako wewe Daudi mutumishi wangu, nitawaokoa watu wangu Waisraeli kutoka Wafilistini na kutoka waadui zao wengine.’ ”


Mungu aniue ikiwa sitatimiza yote ambayo Yawe alimwapia Daudi.


Halafu Samweli akamwambia Saulo: “Tangu leo Yawe ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako na atamupa mutu mwingine kati ya wajirani zako anayekuwa bora kuliko wewe.


“Mwisraeli yeyote, mwanaume au mwanamuke, hatakuwa hata kidogo kahaba wa kidini.


Goliati akamwuliza Daudi: “Sasa, hiyo fimbo ni ya nini? Unazani mimi ni imbwa hata unifikie kwa fimbo?” Mufilistini yule akamulaani Daudi kwa miungu yake.


Abeneri mwana wa Neri, mukubwa wa waaskari wa Saulo alikuwa amemukamata Isiboseti mwana wa Saulo na kumupeleka kule Mahanaimu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite