Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 3:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Ijapokuwa mumenipakaa mafuta kusudi nikuwe mufalme, lakini leo mimi ni zaifu. Hawa wana wa Zeruya ni wakali kupita kipimo. Yawe awaazibu waovu hawa sawasawa na uovu wao.”

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 3:39
30 Referans Kwoze  

Siku kwa siku nitawaangamiza waovu wote katika inchi; nitawaangamiza wabaya wote katika muji wa Yawe.


Uwalipe kwa kadiri ya matendo yao, kufuatana na maovu waliyotenda. Uwalipe kwa kadiri ya matendo yao wenyewe; uwatendee yale wanayostahili.


Alesanduro, yule mufua vyuma amenitendea mabaya mengi. Bwana atamulipa kufuatana na matendo yake.


maana yeye anamutumikia Mungu kwa faida yako. Lakini kama ukifanya mabaya, umwogope kwa sababu yeye yuko na uwezo kwa kuazibu. Yeye anamutumikia Mungu wa kuazibu wale wanaofanya mabaya.


Uwaondoe waovu mbele ya mufalme, na utawala wake utaimarika katika haki.


Mungu amesema mara na mara, nami nimesikia tena na tena kwamba uwezo ni wa Mungu.


Umwambie akuwe macho, atulie na asiogope wala asivunjike moyo, kwa sababu ya hasira kali ya mufalme Resini wa Aramu, na ya mwana wa Remalia. Hao wawili ni kama tu moshi wa kuni zinazozimika.


Mufalme anapoikaa kwa kutoa hukumu, anapepeta uovu wote kwa macho yake.


Lakini mimi nitafurahi milele, nitamwimbia Mungu wa Yakobo sifa.


Anachimba shimo, na kulirefusha, kisha anatumbukia humo yeye mwenyewe.


Daudi akajisemesha: “Nyumba ambayo mwana wangu Solomono atakayomujengea Yawe itakuwa nzuri sana, ya kusifiwa na tukufu katika dunia yote. Lakini kwa vile yeye bado angali kijana na bado hana maarifa mengi, afazali nimufanyie matayarisho.” Hivyo basi, Daudi akaweka akiba kubwa sana ya vitu vya kujenga mbele ya kufa kwake.


Ninyi ni wandugu zangu, ninyi ni damu yangu. Kwa nini mukuwe wa mwisho kunirudisha mimi mufalme kwangu?


Anayepiga mutu na kumwua, hakika anapaswa kuuawa.


Mufalme Daudi aliwaambia watumishi wake: “Hamujui kwamba leo mukubwa na mutu wa heshima amekufa katika inchi ya Israeli?


Lakini mufalme akamwambia: “Kuna maneno gani kati yangu na ninyi wana wa Zeruya? Ikiwa Yawe amemwambia: ‘Umulaani Daudi’, nani sasa anaweza kuuliza: ‘Kwa nini umefanya hivyo?’ ”


Halafu Abisayi mwana wa Zeruya akasema: “Si Simei anapaswa kuuawa maana alimulaani muchaguliwa wa Yawe?”


Mungu atamwazibu Yoabu kwa mauaji hayo aliyoyafanya bila baba yangu kuwa na habari. Yeye aliwaua watu wawili ambao walikuwa wa maana zaidi kuliko yeye, tena walimupita kwa wema; aliwaua Abeneri mwana wa Neri, jemadari wa kundi la waaskari Waisraeli, na Amasa mwana wa Yeteri, jemadari wa waaskari wa Yuda.


Mufalme Daudi akawaambia wale watu wote waliokusanyika: “Solomono mwana wangu, ambaye peke yake amechaguliwa na Mungu, angali bado mudogo, hana maarifa mengi na kazi hii ni kubwa. Nyumba atakayojenga si ya mwanadamu, lakini ni ya Mungu, Yawe.


Na watu wa ovyoovyo wakajiunga naye, watu wapumbafu wasiofaa kitu, nao wakamushawishi Rehoboamu mwana wa Solomono kutenda yale waliyotaka wao, naye hangeweza kuwazuia maana wakati ule alikuwa angali kijana bila mazoezi mengi.


Mufalme Zedekia akasema: Basi! Mutu huyu yuko katika mikono yenu; mimi siwezi kuwapinga.


Wale watu kwa pamoja wakamwendea mufalme Dario na kumwambia: Ee mufalme, ujue kwamba hakuna sheria wala amri yoyote ya Wamedi na Wapersi inayoweza kubadilishwa kisha kuwekwa na mufalme.


Lakini ninawaonya kwamba musipotimiza ahadi yenu, mutakuwa mumemutendea Yawe zambi; mujue kwa hakika kwamba mutaazibiwa.


Vilevile Mungu akawafanya watu wa Sekemu waazibiwe kwa uovu wao walioufanya. Hivyo, laana ya Yotamu mwana wa Yerubali ikawapata.


Lakini wewe usimwache bila kumwazibu. Una hekima, utajua utakalomufanyia. Ingawa yeye ana imvi, usimwache. Umwue ingawa ni muzee.”


Lakini ole kwao watu waovu! Mambo yatawaendekea vibaya, maana yale waliyotenda yatawapata wao wenyewe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite