Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 24:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kwa mara nyingine, Yawe aliwakasirikia Waisraeli, akamusukuma Daudi kuwatendea vibaya, akamwambia awahesabu watu wa Israeli na watu wa Yuda.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 24:1
23 Referans Kwoze  

Shetani akaenda kinyume cha Waisraeli, akamushawishi Daudi kuwahesabu watu.


Hivi walitimiza mambo uliyokuwa umekusudia tangu zamani kwa uwezo wako na kwa mapenzi yako.


Tena niliwapa masharti mabaya na maagizo ambayo hayawezi kuwawezesha kuishi.


Na ikiwa nabii yule akidanganyika na kusema kitu, basi mimi Yawe nimemupotosha. Nami nitanyoosha mukono wangu kwa kumwondoa nabii yule kutoka kwa watu wangu Waisraeli.


Lakini mufalme akamwambia: “Kuna maneno gani kati yangu na ninyi wana wa Zeruya? Ikiwa Yawe amemwambia: ‘Umulaani Daudi’, nani sasa anaweza kuuliza: ‘Kwa nini umefanya hivyo?’ ”


Sikiliza, Yawe anasema: ‘Nitaleta hasara katika jamaa yako mwenyewe. Nitawatwaa wake zako ukiona kwa macho yako mwenyewe na kumupa jirani yako, naye atalala nao waziwazi.


Basi, sasa bwana wangu mufalme, usikie maneno ya mutumishi wako. Ikiwa Yawe ndiye aliyekuchochea ukuje kunishambulia, basi, apokee sadaka ambayo itamusukuma kubadilisha mawazo yake. Lakini ikiwa ni watu, basi, Yawe awalaani watu hao maana wamenifukuza kutoka urizi ambao Yawe aliotupa wakisema: ‘Kwenda uitumikie miungu mingine.’


Lakini nitafanya moyo wa mufalme kuwa mugumu. Na hata kama nitazidisha vitambulisho na maajabu yangu katika inchi ya Misri,


Ninyi mulitaka kunitendea vibaya, lakini Mungu alikusudia mema kusudi watu wengi wapate kuwa wazima kama vile munavyoona leo.


Lakini sasa musifazaike wala kuhuzunika kwa kuniuzisha. Mungu ndiye aliyenileta huku niwatangulie, kusudi niyaokoe maisha ya watu.


Kwa sababu hii Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu wapate kuamini mambo ya uongo.


Kisha Musa akamwambia Haruni na wana wake, Eleazari na Itamari: Musivuruge nywele zenu wala musipasue nguo zenu kwa kuomboleza, kama sivyo mutakufa na kuwaletea Waisraeli wote pamoja kasirani ya Yawe. Lakini wandugu zenu, ni kusema jamii yote ya Israeli, wanaweza kuomboleza kwa sababu ya moto huo Yawe alioleta.


kama vile Yawe alivyomwamuru Musa. Musa akawahesabu watu hawa kule katika jangwa la Sinai.


Wana wa Tola walikuwa: Usi, Refaya, Yerieli, Yamai, Ibusamu na Semweli. Hao walikuwa wakubwa wa jamaa za ukoo za Tola na watu mashujaa sana wa vita nyakati zao. Hesabu ya wazao wao siku za utawala wa mufalme Daudi ilikuwa elfu makumi mbili na mbili na mia sita.


Basi, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Israeli, naye akawaacha wanyanganyi wanyanganye mali zao. Akawatoa kwa waadui zao waliowazunguka hata wasiweze tena kuwashinda.


Kwa hiyo Yawe akawaka hasira juu ya Waisraeli, akasema: “Kwa sababu watu hawa wamevunja agano nililofanya na babu zao, wakakataa kutii sauti yangu,


Kwa hiyo mufalme Yoramu akaondoka Samaria, akakusanya waaskari wote wa Israeli.


Hao wote walikuwa wazao wa Aseri na walikuwa wakubwa wa jamaa zao, watu wafundi na hodari wa vita. Hesabu ya wale walioandikwa kwa kufuata ukoo katika kundi la waaskari ilikuwa elfu makumi mbili na sita.


Lakini Hezekia hakumutolea Yawe shukrani kwa yale yote aliyomutendea kwa sababu moyo wake ulikuwa umejaa majivuno. Hii ikasababisha kutaabika kwa inchi ya Yuda na Yerusalema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite