Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 22:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ninamwita Yawe anayestahili sifa anisaidie, nami ninaokolewa kutoka kwa waadui zangu.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 22:4
20 Referans Kwoze  

Yawe ni kikingio changu, kimbilio langu, mukombozi wangu, Mungu wangu, yule ambaye ninamukimbilia, ngao yangu, nguvu ya wokovu wangu, munara wangu.


Nao waliimba hivi kwa sauti kubwa: “Mwana-Kondoo aliyeuawa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima na nguvu, heshima, utukufu na sifa!”


Ni kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Kila mutu anayemusihi Bwana, ataokolewa.”


Yeye amenitegea sikio, hivyo nitamwomba muda wote wa maisha yangu.


Maana Yawe ni mukubwa, anasifiwa sana; anastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.


“Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili utukufu, heshima na uwezo, kwa maana wewe ndiwe uliyeumba vitu vyote; vile vimeumbwa na kupata kuwa kutokana na mapenzi yako.”


Nitakutolea sadaka za shukrani. Nitaomba kwa jina la Yawe.


Nitamutolea sadaka ya divai kwa kumushukuru maana ameniokoa. Nitaomba kwa jina la Yawe.


Kisha nikamulilia Yawe: “Ee Yawe, tafazali uniokoe!”


Ni nani anayeweza kutaja matendo ya Yawe? Ni nani anayeweza kumusifu kama anavyostahili?


Muimbe kwa ajili ya utukufu wa jina lake, mumusifu kwa utukufu!


Wewe unajua kutangatanga kwangu; unaweka machozi yangu ndani ya chupa. Yote yanakuwa katika kitabu chako.


Acha kifo kiwashitukie waadui zangu, washuke chini katika kuzimu wangali wazima; maana uovu umejaa katika mioyo yao.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Mumugeukie Mungu mupate kufurahi; nanyi hamutafezeheka hata kidogo.


Walawi, ni kusema Yesua, Kadimieli, Bani, Hasabuea, Serebia, Hodia, Sebania na Petahia, wakawaambia watu: Musimame na kumusifu Yawe, Mungu wenu. Mumusifu milele na milele! Na watu wakasifu jina lako tukufu, ambalo linatukuka kuliko baraka na sifa zote.


Wakati walipoanza kuimba na kusifu, Yawe akawavuruga akili waaskari Waamoni, Wamoabu na watu wa mulima Seiri waliokuja kupigana na Yuda. Na waaskari wale wakashindwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite