Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 21:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Basi, utupatie watu saba kati ya wazao wake, nasi tuwatundike mbele ya Yawe juu ya mulima Gibea, kwa Saulo aliyechaguliwa na Yawe.” Mufalme akasema: “Nitawapatia nao.”

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 21:6
22 Referans Kwoze  

Samweli akawaambia watu wote: “Huyu ndiye mutu aliyechaguliwa na Yawe kati ya watu wote; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye.” Watu wote wakapiga kelele: “Mufalme aishi milele.”


Wale wajumbe walipofika katika muji wa Gibea, ambako Saulo alikoishi, wakaeleza habari hizo na watu wote wakaanza kulia kwa sauti.


Vilevile, Saulo pamoja na wapiganaji hodari ambao zamani Mungu aligusa mioyo yao, alikwenda kwake kule katika muji wa Gibea.


Na kisha wakaomba wapewe mufalme. Kwa hiyo Mungu akawawekea Saulo, mwana wa Kisi, wa kabila la Benjamina kwa kuwatawala kwa muda wa miaka makumi ine.


Yuda akatupa vile vikoroti ndani ya hekalu, naye akaondoka na kwenda kujitundika.


wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedata, adui ya Wayuda. Hata hivyo, hawakunyanganya mali zao.


Ninaamuru vilevile kwamba mutu yeyote ambaye hatatii amri hii, muti mumoja uongolewe kutoka katika nyumba yake na atundikwe juu yake. Tena, nyumba yake ifanywe kuwa yalala.


Mutu mumoja aliyeona tukio hilo, akamwambia Yoabu: “Nimemwona Abusaloma akilembelea kwenye muti wa mwalo.”


Ahitofeli alipoona kwamba shauri lake halikufuatwa, alitandika punda wake, akaenda kwake, kwenye muji wake. Alipofika kule, alipanga vizuri mambo ya nyumba yake, akajitundika. Akakufa na kuzikwa kwenye kaburi la baba yake.


Halafu Samweli akatwaa chupa ndogo ya mafuta akamumiminia Saulo juu ya kichwa, akamubusu na kumwambia: “Yawe amekutia mafuta ukuwe mutawala juu ya watu wake.


Kisha, Yoshua aliwanyonga kwa kuwatundika kwenye miti mitano ambako walitundikwa mpaka magaribi.


Kisha akamutundika mufalme wa Ai juu ya muti wa tini mpaka magaribi. Lakini jua lilipoanza kutua, Yoshua aliamuru maiti yake iondolewe juu ya muti na kutupwa kwenye mulango wa muji kisha walundike lundo kubwa la mawe juu ya maiti hiyo. Lundo hilo liko kule mpaka leo.


“Kama mutu amefanya kosa linalomupasa auawe na akiuawa kwa kutundikwa juu ya muti,


Lakini yule mupishi mukubwa wa mikate akamutundika juu ya muti, kama vile Yosefu alivyokuwa amewaelezea ndoto zao.


Nyuma ya siku tatu mufalme atakunyanyua kutoka katika kifungo, atainua kichwa chako kusudi akutundike juu ya muti, nao ndege watakula mwili wako.”


Sasa nimejua kwamba hakika utakuwa mufalme wa Israeli, na ufalme wa Israeli utaimarishwa chini yako.


Sasa, amenisingizia kwako, ee bwana wangu mufalme. Lakini wewe, bwana wangu mufalme, uko kama malaika wa Mungu. Fanya sawa unavyotaka.


Lakini uniapie kwa jina la Yawe kwamba hautawateketeza wazao wangu, wala kufuta kabisa jina langu katika jamaa ya baba yangu.”


Kiongozi wao alikuwa Ahiezeri aliyesaidiwa na Yoasi, wote wawili ni wana wa Sema kutoka Gibea, Yezieli na Peleti, wana wa Azimaweti, Beraka na Yehu kutoka Anatoti, Isimaya kutoka Gibeoni aliyekuwa mutu shujaa kati ya wale makumi tatu na kiongozi wao, Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi kutoka Gedera, Elizai, Yeremoti, Bealia, Semaria, na Sefatia wa muji wa Harufi, Elekana, Isia, Azareli, Yoezeri, Yasobeamu kutoka ukoo wa Kora, Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite