Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 20:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yoabu akamwambia Amasa: “Habari gani ndugu yangu?” Yoabu akamushika Amasa kwenye kidevu kwa mukono wa kuume sawa vile anataka kumubusu.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 20:9
14 Referans Kwoze  

Hakuna mutu mwaminifu kwa Mungu aliyebaki katika inchi, hakuna mutu yeyote mwenye usawa kati ya watu. Kila mumoja anavizia kumwanga damu; kila mumoja anamwinda mwenzake kusudi amunase.


Mwenzangu amemushambulia rafiki yake, amevunja mapatano yake.


Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.


Zaidi ya hayo, Abusaloma alinyoosha mukono wake akamukumbatia na kumubusu mutu yeyote aliyekuja kuinama mbele yake.


Wakati ule, Abusaloma alikuwa amemuweka Amasa kuwa jemadari wa waaskari pahali pa Yoabu. Amasa alikuwa mwana wa Itira, Mwisimaeli. Mama yake aliitwa Abigaili binti wa Nahasi, aliyekuwa dada ya Zeruya mama ya Yoabu.


Mufalme akamwambia: “Kijana Abusaloma ni muzima?” Ahimasi akasema: “Wakati Yoabu aliponituma mimi mutumishi wako, niliona kulikuwa kelele nyingi, lakini sikufahamu maana yake.”


Mungu atamwazibu Yoabu kwa mauaji hayo aliyoyafanya bila baba yangu kuwa na habari. Yeye aliwaua watu wawili ambao walikuwa wa maana zaidi kuliko yeye, tena walimupita kwa wema; aliwaua Abeneri mwana wa Neri, jemadari wa kundi la waaskari Waisraeli, na Amasa mwana wa Yeteri, jemadari wa waaskari wa Yuda.


Isimaeli mwana wa Netania pamoja na wale watu kumi, wakasimama na kumushambulia kwa upanga Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, wakamwua. Gedalia ndiye aliyekuwa amesimikwa na mufalme wa Babeli kuwa mutawala wa inchi.


Lakini Waisraeli walipomulilia Yawe, basi, aliwapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Ehudu, mwana wa Gera wa kabila la Benjamina. Alikuwa mwenye kutumikisha zaidi mukono wa kushoto. Waisraeli wakamutuma apeleke zawadi zao kwa Mwana-Ngombe, mufalme wa Moabu.


Kama vile rangi yenye kungaa iliyopakwa juu ya chungu cha udongo, ndivyo maneno matamu yenye nia mbaya yanavyokuwa.


Makaripio ya rafiki yanaonyesha uaminifu, lakini busu la adui ni udanganyifu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite