Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 19:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mufalme Daudi akatuma ujumbe kwa makuhani Zadoki na Abiatari: “Muwaambie wazee wa Yuda: ‘Kwa nini ninyi ndio mutakuwa wa mwisho kumurudisha mufalme katika nyumba yake? Maneno yote Waisraeli waliyosema yamenifikia mimi mufalme.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 19:12
9 Referans Kwoze  

Kisha makabila yote ya Waisraeli yalimwendea Daudi kule Hebroni, na kumwambia: “Angalia, sisi ni mwili na damu yako.


kwa sababu sisi ni viungo vya mwili wake.


“Museme hapa hapa mbele ya wanainchi wote wa Sekemu: Jambo gani ni jema kwenu, kwamba watoto wote makumi saba wa kiume wa Yerubali wawatawale au mutoto mumoja? Mukumbuke kwamba mimi ni damu yenu.”


Halafu huyo mwanaume akasema: “Kweli! Huyu ni mufupa kutoka mifupa yangu, na nyama kutoka nyama yangu. Huyu ataitwa ‘Mwanamuke’, kwa sababu ametolewa katika mwanaume.”


Kwa sababu hii ninaweza kuwafanya watu wa taifa langu wawasikilie wivu, hata nipate kuwaokoa wamoja kati yao.


Naye Labani akasema: “Hakika, wewe ni jamaa yangu, damu moja nami!” Yakobo akakaa naye kwa muda wa mwezi mumoja.


Mufalme aliendelea mpaka Gileadi. Kimuhamu akakuwa anafuatana naye. Watu wote wa Yuda na nusu ya watu wa Israeli walikuwa wakimusindikiza mufalme.


Kisha, watu wote wa Israeli wakakuja kwa mufalme na kumwambia: “Kwa nini wandugu zetu watu wa Yuda walikuwa wamekutwaa ukiwa katika njia, wakakuvukisha muto Yordani, wewe na jamaa yako, pamoja na watu wako?”


Zadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiatari walikuwa makuhani. Seraya alikuwa katibu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite