Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 19:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Hapo mufalme alishikwa na huzuni kubwa, akapanda kwenye chumba kilichokuwa juu ya mulango na kulia. Alipokuwa anapanda, alilia akisema: “Mwana wangu Abusaloma, mwana wangu Abusaloma! Ingekuwa heri ningalikufa pahali pako! Ole, Abusaloma mwana wangu! Mwana wangu!”

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 19:1
9 Referans Kwoze  

Yoabu akamwambia: “Mimi sina wakati wa kupoteza pamoja nawe.” Yoabu akatwaa mikuki midogo mitatu katika mukono wake, akaenda na kumuchoma Abusaloma ndani ya moyo, Abusaloma akiwa angali muzima kwenye tawi la muti wa mwalo.


Mufalme akawaamuru Yoabu, Abisayi na Itayi: “Kwa ajili yangu, mumutendee yule kijana Abusaloma kwa upole.” Watu wote walimusikia mufalme alipoamuru wakubwa wake juu ya Abusaloma.


Mutoto mupumbafu ni huzuni kwa baba yake, na uchungu kwa mama yake muzazi.


Yoabu akamwambia: “Leo, hautapeleka habari hiyo. Unaweza kupeleka habari hizo siku nyingine. Lakini leo hautapeleka habari zozote kwa sababu mwana wa mufalme amekufa.”


Lakini yule mutu akamwambia Yoabu: “Hata kama ningeuona uzito wa vikoroti elfu moja vya feza katika mukono wangu, singeunyoosha mukono wangu juu ya mwana wa mufalme kwa kumwua. Maana, tulimusikia mufalme alipokuamuru wewe Abisayi na Itayi, kwamba kwa ajili yake, mumulinde kijana Abusaloma.


Yoabu alipata habari kwamba mufalme alikuwa akilia na kuomboleza juu ya kifo cha Abusaloma.


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


Watoto wake wanaume na wanawake wakamufikia kwa kumufariji, lakini akakataa kufarijiwa, akisema: “Uniache. Nitaendelea kuomboleza kwa ajili ya mwana wangu, mpaka nitakaposhuka katika kaburi.” Ndivyo baba yake alivyomulilia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite