Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 16:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kwa hiyo, Abisayi mwana wa Zeruya akamwambia mufalme: “Kwa nini huyu anayekuwa sawa imbwa mufu akulaani wewe bwana wangu mufalme? Uniruhusu nimwendee, nami nitakikata kichwa chake.”

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 16:9
13 Referans Kwoze  

Usikawie kunitolea sehemu yangu kutokana na wingi wa mazao yako na divai yako. Mutanipa wazaliwa wenu wa kwanza wanaume.


Mefiboseti akainama, na kusema: “Mimi ni sawa na imbwa mufu. Kwa nini unishugulikie hivyo?”


Abeneri alikasirika sana kutokana na maneno ya Isiboseti, akasema: “Unafikiri mimi ni imbwa anayeitumikia jamaa ya Yuda? Angalia, mimi nimewatendea mema jamaa ya baba yako Saulo, wandugu zake, na warafiki zake na sikukutoa kwa Daudi mpaka leo. Hata hivyo, leo hii unaniona kuwa mwenye kosa kwa ajili ya mwanamuke.


Kumbuka mezali ya kale inayosema ‘Uovu unatoka ndani ya mwovu’, lakini sitanyoosha mukono juu yako.


Muwaheshimu watu wote. Muwapende wandugu zenu waamini. Mumwogope Mungu, mumuheshimu mufalme.


Paulo akasema: “Wandugu zangu, sikujua kwamba yeye ni Kuhani Mukubwa. Kwa maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Usimulaani mukubwa wa taifa lako.’ ”


Wanafunzi wake, Yakobo na Yoane walipoona mambo hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuombe moto uwashukie toka mbinguni na kuwateketeza?”


Yoabu na ndugu yake Abisayi walimwua Abeneri kwa sababu alikuwa amemwua ndugu yao Asaeli wakati wa vita kule Gibeoni.


Maana, mimi mutumishi wako ninajua kwamba nilitenda zambi. Hii ndiyo sababu nimekuja leo, nikiwa wa kwanza katika kabila la Yosefu kuja kukupokea wewe bwana wangu, mufalme.”


Halafu Abisayi mwana wa Zeruya akasema: “Si Simei anapaswa kuuawa maana alimulaani muchaguliwa wa Yawe?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite