Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 16:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Yawe amekulipiza kisasi kutokana na kumwanga damu ya watu wote wa jamaa ya Saulo, ambaye sasa wewe umenyanganya ufalme kwa pahali pake. Sasa, Yawe amemupa mwana wako Abusaloma ufalme. Maangamizi yamekupata kwa sababu wewe ni mwuaji.”

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 16:8
18 Referans Kwoze  

Daudi akasema: “Ubebe wewe mwenyewe lazima ya kifo chako, maana umejishuhudia wewe mwenyewe kwa kinywa chako mwenyewe ukisema: ‘Nimemwua muchaguliwa wa Yawe.’ ”


Ndivyo watu wa Sekemu pamoja na ndugu yao Abimeleki walivyoazibiwa kwa sababu waliwatendea kwa ukali wana makumi saba wa Yerubali. Azabu ya mauaji hayo iliwapata maana Abimeleki aliwaua akisaidiwa na hao watu wa Sekemu.


Watu hawa walimwanga damu ya watu wako na ya manabii wako, kwa sababu hiyo sasa umewakunywesha damu, nao wanastahili kutendewa vile!”


Ee Mungu, muteteaji wa haki yangu, unijibu ninapoomba. Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia; unionee huruma na kusikia maombi yangu.


Ee Yawe, angalia ginsi waadui zangu wanavyokuwa wengi. Ni wengi sana hao wanaonishambulia.


Daudi aliwatoa watoto hao saba wanaume kwa Wagibeoni, nao wakawatundika kwenye mulima mbele ya Yawe, wote saba wakakufa pamoja. Watoto hao waliuawa kwa mwanzo wa mavuno ya Shayiri.


Maana, mimi mutumishi wako ninajua kwamba nilitenda zambi. Hii ndiyo sababu nimekuja leo, nikiwa wa kwanza katika kabila la Yosefu kuja kukupokea wewe bwana wangu, mufalme.”


Wakati mumoja katika siku za utawala wa Daudi kukatokea njaa kali katika inchi. Njaa hiyo ilidumu miaka mitatu yenye kufuatana. Daudi alimwomba Yawe shauri. Yawe akamwambia: “Saulo na jamaa yake wana makosa ya kumwanga damu kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”


Unisikilize na kunijibu; nimechoka na malalamiko yangu.


Basi, wakavuka kwenye kivuko kwa kuisindikiza jamaa ya mufalme na kumufanyia mufalme yote aliyoyapenda. Simei mwana wa Gera akakuja, akajitupa mbele ya mufalme, akainama uso mpaka chini, wakati mufalme alipokuwa karibu kuvuka muto Yordani.


Vilevile, kuko Simei mwana wa Gera, wa kabila la Benjamina wa muji wa Bahurimu, ambaye aliniapiza na kunilaani vikali nilipokwenda kule Mahanaimu; lakini alipokuja kunipokea kwenye muto Yordani, nilimwapia kwa jina la Yawe nikimwambia: ‘Sitakuua kwa upanga.’


Ee Yawe, Mungu wangu! Kama nimetenda moja ya mambo haya: kama nimechafua mikono yangu kwa ubaya,


Kama vile ndege anavyorukaruka, vilevile laana isiyokuwa na sababu haimupati mutu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite