Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 16:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Wakati Daudi alipofika kule Bahurimu, kulitokea mutu mumoja wa ukoo wa Saulo, jina lake Simei mwana wa Gera, akaanza kumulaani Daudi kwa mufululizo.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 16:5
22 Referans Kwoze  

Lakini Paltieli akaenda pamoja na muke wake akiwa analia njia yote mpaka kule Bahurimu. Abeneri akamwambia Paltieli: “Rudia kwako.” Naye akarudi.


Goliati akamwuliza Daudi: “Sasa, hiyo fimbo ni ya nini? Unazani mimi ni imbwa hata unifikie kwa fimbo?” Mufilistini yule akamulaani Daudi kwa miungu yake.


Usikawie kunitolea sehemu yangu kutokana na wingi wa mazao yako na divai yako. Mutanipa wazaliwa wenu wa kwanza wanaume.


Lakini wakati huu, walionekana na kijana mumoja ambaye alikwenda na kumupasha Abusaloma habari. Kwa hiyo, Yonatani na Ahimasi waliondoka haraka, wakaenda Bahurimu katika nyumba ya mutu fulani aliyekuwa na kisima katika kiwanja chake. Wakaingia ndani ya kisima na kujificha.


Watu watatangatanga katika inchi, wenye kufazaika sana na wenye njaa. Na wakiwa na njaa, watakasirika na kumulaani mufalme wao vilevile na Mungu wao. Wataangalia juu mbinguni


Usimutukane mutawala hata ndani ya moyo wako, wala usimutukane tajiri hata ndani ya chumba chako cha kulala, maana ndege atapeleka sauti yako, kiumbe kinachoruka kitatangaza maneno yako.


Kama vile ndege anavyorukaruka, vilevile laana isiyokuwa na sababu haimupati mutu.


Uwaache walaani, lakini wewe unibariki; wanaonishambulia wafezeheke, nami mutumishi wako nifurahi.


Kambi zao ziachwe matongo, mutu yeyote asiishi katika mahema yao.


Kisha mufalme pamoja na watu wote waliokuwa pamoja naye, wakafika kwenye muto wakiwa wamechoka. Basi wakapumzika.


Mufalme akamwambia Siba: “Basi, yale yaliyokuwa mali ya Mefiboseti sasa ni mali yako.” Siba akamwambia: “Ninashukuru, bwana wangu mufalme, nami ninaomba nipate kukubaliwa mbele yako siku zote.”


Akakuwa anamutupia mufalme Daudi pamoja na watumishi wake mawe ingawa watu wengine wote na mashujaa walikuwa wakimuzunguka Daudi upande wa kuume na wa kushoto.


Ninalala macho wazi, kama ndege anayekuwa peke yake juu ya paa.


Usimutukane Mungu, wala kumulaani mukubwa wa watu wako.


Abialboni wa muji Araba; Azimaweti wa muji Bahurimu;


Katika muji wa Susani, kulikuwa mutu mumoja Muyuda, jina lake Mordekayi, mwana wa Yairi wa uzao wa Simei, na Kisi wa kabila la Benjamina.


Kwa maana Mungu ameniregeza na kunishusha, wamekuwa huru kunitendea wanavyopenda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite