5 Zaidi ya hayo, Abusaloma alinyoosha mukono wake akamukumbatia na kumubusu mutu yeyote aliyekuja kuinama mbele yake.
Kwa hiyo Yoabu akaenda na kumwelezea mufalme maneno hayo yote, naye akamwita Abusaloma. Abusaloma akaingia kwa mufalme, akaanguka uso mpaka chini mbele ya mufalme. Na mufalme akamubusu Abusaloma.
Akisema maneno mazuri usimwaminie. Ndani ya moyo wake kuna machukizo mengi.
Mwenzangu amemushambulia rafiki yake, amevunja mapatano yake.
Wewe haukunibusu kwa kunisalimia, lakini mwanamuke huyu hakuacha kubusu miguu yangu tangu nilipoingia humu.
Yoabu akamwambia Amasa: “Habari gani ndugu yangu?” Yoabu akamushika Amasa kwenye kidevu kwa mukono wa kuume sawa vile anataka kumubusu.