Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 15:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Abusaloma alimwambia: “Maneno yako ni ya haki kabisa. Lakini hakuna mutu yeyote aliyechaguliwa na mufalme kwa kukusikiliza.”

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 15:3
16 Referans Kwoze  

Na zaidi atawaazibu wale wanaoishi kufuatana na tamaa mbaya za kimwili na kuzarau mamlaka ya Mungu. Walimu wale wa uongo ni wenye kiburi, wenye kujivuna, nao hawaogopi kutukana viumbe vitukufu vya mbinguni.


Muwaheshimu watu wote. Muwapende wandugu zenu waamini. Mumwogope Mungu, mumuheshimu mufalme.


Paulo akasema: “Wandugu zangu, sikujua kwamba yeye ni Kuhani Mukubwa. Kwa maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Usimulaani mukubwa wa taifa lako.’ ”


Kwa maana Mungu alisema: ‘Uwaheshimu baba yako na mama yako.’ Naye alisema vilevile: ‘Anayelaani baba yake au mama yake anapaswa kuuawa.’


Mufalme atakayefuata atakuwa wa kuzarauliwa ambaye asiyeweza kupewa heshima ya kifalme, naye atakuja wakati watu wasiouzania na kunyanganya ufalme kwa werevu.


Kwako baba na mama wanazarauliwa. Mugeni anayekaa kwako ananyanganywa mali yake. Wayatima na wajane wanaonewa.


Kama mutu akimuchekelea baba yake na kuzarau utii kwa mama yake, macho yake yataondolewa na kibombobombo wa pori na kuliwa na tai.


Kuna watu ambao wanalaani baba zao, wala hawana shukrani kwa mama zao.


Mutu muzuri anapata rehema za Yawe, lakini mwenye nia mbaya analaaniwa na Mungu.


Unisaidie, ee Yawe! Watu wema wamekwisha; waaminifu wametoweka kati ya watu.


Kwa hiyo, Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akawahukumu watu wake wote kufuatana na haki na sheria.


Wakakusanyika mbele ya Musa na Haruni, wakawaambia: Ninyi mumepitisha kipimo! Waisraeli wote pamoja ni watakatifu; kila mumoja ni mutakatifu. Yawe yuko pamoja nasi wote. Mbona sasa ninyi munajifanya wakubwa kushinda watu wengine wa Yawe?


Anayemulaani baba yake au mama yake hakika atauawa.


Uwaheshimu baba yako na mama yako, kusudi uishi maisha marefu katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Tena, Abusaloma alimwambia: “Ingekuwa heri mimi ningekuwa mwamuzi wa Waisraeli! Kila mutu mwenye mashitaki au shauri angekuja kwangu, nami ningemupa haki yake!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite