Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 15:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Basi, mufalme akaondoka pamoja na jamaa yake, lakini akawaacha wahabara wake kumi wakishugulika na kazi za nyumba.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 15:16
12 Referans Kwoze  

Zaburi ya Daudi. Inaelekea wakati alipomukimbia mwana wake Abusaloma.


Nyuma, Daudi alifika katika nyumba yake kule Yerusalema. Mufalme aliwatwaa wahabara wake kumi ambao alikuwa amewaacha kwa kuangalia nyumba yake, akawaweka kwenye nyumba moja wapate kulindwa, akawatunza vizuri, lakini hakulala nao. Kwa hiyo wahabara hao wakakuwa wakifungwa mpaka siku za kufa kwao, wakaishi kama vile walikuwa wajane.


Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.


Sikiliza, Yawe anasema: ‘Nitaleta hasara katika jamaa yako mwenyewe. Nitawatwaa wake zako ukiona kwa macho yako mwenyewe na kumupa jirani yako, naye atalala nao waziwazi.


Abigaili alifanya haraka, akasimama na kupanda juu ya punda wake, akifuatana na wajakazi wake watano, akaenda na watumishi wa Daudi. Akakuwa muke wake.


Bwana wangu, ninakuomba upokee zawadi hii niliyokuletea, na uwape vijana wanaokufuata.


Baraka akayaita makabila ya Nafutali na Zebuluni kule Kedesi. Watu elfu kumi wakamufuata. Debora akaenda pamoja naye.


Watumishi wake wakamwambia: “Sisi watumishi wako, bwana wetu mufalme, tuko tayari kufanya neno lolote unaloamua.”


Mufalme akaondoka pamoja na watu wake wote. Lakini akasimama kidogo walipofikia nyumba ya mwisho katika muji.


Yule tajiri alikuwa na kondoo wengi na ngombe wengi.


Watu wote walikuwa wanabishana wao kwa wao katika makabila yote ya Israeli, wakisema: “Mufalme Daudi alitukomboa toka mikono ya waadui zetu, alituokoa toka mikono ya Wafilistini. Lakini sasa ameikimbia inchi, akimukimbia Abusaloma.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite