Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 15:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Lakini Abusaloma alituma wajumbe kwa siri katika makabila yote ya Waisraeli, wakasema: “Mara moja mutakaposikia mulio wa baragumu, museme: ‘Abusaloma ni mufalme katika Hebroni!’ ”

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 15:10
16 Referans Kwoze  

Kutoka kabila la Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase kutoka ngambo ya muto Yordani: watu elfu mia moja na makumi mbili wenye kila aina ya silaha za vita.


Siku kwa siku, watu walijiunga na Daudi kwa kumusaidia, na nyuma akakuwa na kundi kubwa sana la waaskari, kama jeshi la Mungu.


Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme kule Hebroni; naye Daudi akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Waisraeli kulingana na neno la Yawe lililotolewa kwa njia ya Samweli.


Mara moja wakubwa wenzake wakavua nguo zao, wakazilundika pamoja kwenye ngazi kusudi asimame juu yake, wakapiga baragumu na kulalamika kwa sauti: “Yehu ni mufalme!”


Halafu umuruhusu kuhani Zadoki na nabii Natani wamupakae mafuta akuwe mufalme wa Israeli. Kisha mupige baragumu na kusema: ‘Mufalme Solomono aishi!’


Watu wote walikuwa wanabishana wao kwa wao katika makabila yote ya Israeli, wakisema: “Mufalme Daudi alitukomboa toka mikono ya waadui zetu, alituokoa toka mikono ya Wafilistini. Lakini sasa ameikimbia inchi, akimukimbia Abusaloma.


Basi, Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Muangalie, Yoabu ana shamba la shayiri karibu na langu. Muende mulichome kwa moto.” Kwa hiyo watumishi wa Abusaloma wakalichoma shamba la Yoabu kwa moto.


Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Mumwangalie Amunoni atakapokuwa amekunywa divai na kufurahi. Nitakapowaambia: ‘Mumupige Amunoni’, mumwue. Hiyo ni amri yangu kwenu. Mujipe moyo na mukuwe hodari.”


Kule Hebroni, alitawala watu wa Yuda kwa muda wa miaka saba na miezi sita, na kule Yerusalema alitawala watu wa Israeli pamoja na Yuda kwa muda wa miaka makumi tatu na mitatu.


Daudi alikuwa mufalme wa kabila la Yuda kwa muda wa miaka saba na nusu, makao yake yalikuwa kule Hebroni.


Nyuma ya mambo yale, Daudi alimwomba Yawe shauri, akasema: “Niende kwenye muji mumoja kati ya miji ya Yuda?” Yawe akamwambia: “Kwenda!” Daudi akamwuliza: “Niende katika muji gani?” Yawe akamujibu: “Kwenda kwenye muji wa Hebroni.”


Mufalme akamwambia: “Basi, kwenda kwa amani.” Abusaloma akaondoka kwenda Hebroni.


Kisha, Natani akamwendea Batiseba mama ya Solomono, akamwuliza: “Haujasikia kwamba Adonia mwana wa Hagiti amejiweka kuwa mufalme na bwana wetu Daudi hana habari?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite