Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 15:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nyuma ya tukio hilo, Abusaloma alijipatia gari, farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 15:1
11 Referans Kwoze  

Wakati ule, Adonia mwana wa Daudi kutoka muke wake Hagiti, akaanza kujivuna kwamba yeye ndiye atakayekuwa mufalme. Basi, akajitayarishia magari, wapanda-farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.


Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua, atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni; kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa.


Sikiliza, Yawe anasema: ‘Nitaleta hasara katika jamaa yako mwenyewe. Nitawatwaa wake zako ukiona kwa macho yako mwenyewe na kumupa jirani yako, naye atalala nao waziwazi.


Samweli aliwaambia: “Hivi ndivyo mufalme wenu atakayewatawala atakavyowatendea: wana wenu atawafanya wakuwe waendeshaji wa magari yake, na wengine kuwa waaskari wapanda-farasi wake, na wengine watapiga mbio mbele ya magari yake.


Anayependa ugomvi anapenda zambi. Anayejivuna anajitafutia maangamizi.


Kiburi kinatangulia maangamizi; majivuno yanatangulia maanguko.


Kiburi kinazaa haya, lakini kwa watu wanyenyekevu kuna hekima.


Naye mufalme akawaambia: “Kwenda na watumishi wangu mimi bwana wako, umupandishe mwana wangu Solomono juu ya nyumbu wangu, umupeleke kule Gihoni.


Hata hivyo, asikuwe na farasi wengi kwa ajili yake mwenyewe, wala asiwarudishe watu Misri kwa kujipatia farasi zaidi, kwa sababu Yawe amewaonya: ‘Hamutarudi tena kwa njia ile.’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite