Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 13:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yonadabu akamwambia Amunoni: “Wewe ni mutoto wa mufalme, kwa nini unakonda na unaonekana hauna furaha kila siku? Mbona hautaki kuniambia?” Amunoni akamwambia: “Ninamupenda Tamari, dada ya ndugu yangu Abusaloma.”

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 13:4
11 Referans Kwoze  

“Musiogope ninyi kundi dogo! Kwa kuwa Baba yenu amependelea kuwapa ninyi ule Ufalme wake.


Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.


Walisikia haya walipotenda machukizo hayo? Hapana, hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka; nitakapowaazibu, wataangamia. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe.


Kama mwanaume yeyote akimwoa dada yake, binti ya baba yake au mama yake na binti huyo akakubaliana na mwanaume huyo ambaye ni kaka yake, na kulala naye, hilo ni chukizo. Wanapaswa kutengwa na watu wao maana wamefanya jambo la haya. Huyo mwanaume atabeba lazima ya uovu wake, maana amelala na dada yake.


Usilale na dada yako, akuwe ni dada yako, binti wa baba yako au wa mama yako hata kama alizaliwa katika nyumba au pahali pengine.


Hapo, Yezebeli, muke wake, akamwambia: “Anayetawala Israeli ni nani? Si ni wewe? Amuka, ukule na uchangamuke. Mimi peke yangu nitakupa shamba la mizabibu la Naboti wa Yezereheli.”


Lakini Amunoni alikuwa na rafiki aliyeitwa Yonadabu, mwana wa Shama, ndugu ya Daudi. Yonadabu alikuwa mutu mwerevu sana.


Yonadabu akamwambia: “Wewe ujilalishe katika kitanda na ujifanye kuwa mugonjwa. Baba yako atakapokuja kukuona, wewe umusihi ukisema: ‘Umuruhusu dada yangu, Tamari, akuje aniletee mukate nipate kula na anitayarishie chakula mbele yangu kusudi nikione naye mwenyewe anikulishe.’ ”


Yezebeli, muke wake, akamwendea na kumwuliza: “Mbona umejaa huzuni ndani ya moyo hata kula haukuli?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite