Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 12:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Natani akamwambia Daudi: “Wewe ndiwe mutu yule! Sasa, Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Mimi nilikupakaa mafuta ukuwe mufalme juu ya Israeli. Nilikuokoa toka katika mikono ya Saulo.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 12:7
22 Referans Kwoze  

Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, naye akawasikilia huruma, akawaponyesha wale waliokuwa wagonjwa kati yao.


Samweli akatwaa pembe lake lenye mafuta akamupakaa Daudi mafuta mbele ya kaka zake. Mara moja roho wa Yawe akamushika Daudi kwa nguvu na kuwa naye tangu siku hiyo. Kisha Samweli akarudi katika muji wa Rama.


Daudi alimwimbia Yawe wimbo huu siku ile Yawe alipomukomboa toka katika mikono wa waadui zake, na toka katika mukono wa Saulo.


Basi, nabii akamwambia mufalme: “Yawe anasema hivi: ‘Umemwachilia akuponyoke mutu ambaye niliamuru auawe. Basi, maisha yake utalipa kwa maisha yako, na watu wake kwa watu wako.’ ”


Elia akamujibu: “Mwenye kutaabisha Waisraeli si mimi, lakini ni wewe na jamaa ya baba yako. Ninyi mumepita pembeni ya amri za Yawe na kuabudu Bali.


Ameniokoa kutoka waadui zangu. Ee Yawe, ulinitukuza juu ya wapinzani wangu na kuniponyesha kutoka watesaji wakali.


Kwa hiyo basi, umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe wa majeshi anasema hivi: Nilikutoa katika shamba la malisho ya nyama ulimokuwa unawachunga kondoo, kusudi ukuwe mukubwa wa watu wangu Waisraeli.


Basi, Daudi alibaki katika makimbilio ndani ya jangwa, katika inchi ya milima ya mbuga za Zifu. Saulo alimutafuta kila siku, lakini Mungu hakumutia Daudi katika mikono yake.


Saulo alipoambiwa kwamba Daudi amekwisha fika Keila, akasema: “Mungu amemutia katika mikono yangu maana amejifungia mwenyewe kwa kuingia katika muji wenye milango yenye vifungio.”


Saulo alifikiri: “Ngoja nitamutoa Mikali kusudi akuwe mutego kwake. Na bila shaka Wafilistini watamwua.” Hivyo Saulo akamwambia Daudi kwa mara ya pili: “Sasa nitakuwa baba mukwe wako.”


Samweli akamwambia: “Ingawa unajiona kwamba wewe ni mudogo, lakini si wewe kiongozi wa makabila ya Israeli? Yawe alikupakaa mafuta kwa kukusimika kuwa mufalme juu ya Israeli.


Samweli akamujibu Saulo: “Umefanya kipumbafu. Haukutii mambo Yawe, Mungu wako, aliyokuamuru. Kama ungetii, Yawe angeudumisha milele ufalme wako juu ya Israeli.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi, mutumishi wa Mungu, aliyomwimbia wakati alipomwokoa katika mikono ya Saulo na waadui wengine.


Basi, alimutupia Daudi mukuki mara mbili maana alifikiri: “Nitamubanisha Daudi kwenye ukuta.” Lakini Daudi aliepa mara zote mbili.


Yule mwanamuke akamwambia: “Kwa nini basi, umepanga kutenda uovu huu juu ya watu wa Mungu? Kulingana na uamuzi wako juu ya jambo hilo, wewe mwenyewe umejihukumu kuwa na kosa kwa sababu haumuruhusu mwana wako arudi kwa nyumba kutoka kule alikokimbilia.


Kwenda umwambie Yeroboamu kwamba Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Nilikuchagua kati ya watu, nikakufanya kiongozi wa watu wangu Waisraeli,


Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu. Utaishi pamoja na nyama wa pori, utakula majani kama ngombe; utalowana na umande wa mbinguni. Utakaa katika hali hiyo kwa miaka saba, na kwa mwisho utatambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya ufalme wa wanadamu naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.


Lakini nilipokuwa nikishugulikashugulika, mutu yule akatoroka.” Mufalme wa Israeli akamwambia: “Ndivyo hukumu yako itakavyokuwa. Umejihukumu mwenyewe.”


Kisha, nabii Yeremia akamwelezea Zedekia, mufalme wa Yuda, maneno hayo yote huko Yerusalema,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite