Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




2 Samweli 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Daudi akapasua nguo yake kwa huzuni. Hata watu waliokuwa pamoja na Daudi wakafanya vilevile.

Gade chapit la Kopi




2 Samweli 1:11
15 Referans Kwoze  

Mufalme Daudi alisimama, akapasua nguo yake kwa huzuni akalala chini. Hata na watumishi wake wote waliokuwa wakisimama karibu naye walipasua nguo zao.


Kisha, mufalme Daudi akamwambia Yoabu na wale wote waliokuwa pamoja naye, wapasue nguo zao, wavae nguo ya gunia kusudi wafanye kilio kwa ajili ya Abeneri. Wakati wa mazishi hayo, mufalme Daudi alitembea nyuma ya kipoyi cha maiti ya Abeneri.


Basi, Rubeni aliporudi kwenye lile shimo, hakumwona Yosefu tena, kwa hiyo akararua nguo zake kwa huzuni,


Halafu Yakobo akararua nguo zake kwa huzuni, akavaa nguo ya gunia katika kiuno. Akamulilia mwana wake kwa muda wa siku nyingi.


Mufurahi pamoja na wenye kufurahi. Mulie pamoja na wenye kulia.


Lakini Barnaba na Paulo waliposikia habari ile, wakapasua nguo zao kwa huzuni, wakaingia haraka katikati ya kundi la watu, na kusema kwa sauti:


Yoshua akapasua nguo yake, yeye pamoja na wazee wa Israeli. Wakajitupa chini ya Sanduku la Yawe mpaka magaribi; wakajitia mavumbi juu ya vichwa vyao.


Kwa hiyo wakararua nguo zao kwa huzuni. Kila mumoja wao akamubebesha punda wake muzigo wake, wakarudi kwa muji.


Basi, Tamari alijipakaa majivu kwenye kichwa, akapasua kanzu yake, akaweka mikono yake juu ya kichwa, halafu akaondoka akiwa analia kwa sauti.


kwa sababu umetubu na kunyenyekea mbele yangu, hata umepasua nguo yako na kulia uliposikia maneno yangu juu ya pahali hapa, na juu ya wakaaji wake, na umejinyenyekeza mbele yangu, nami vilevile nimekusikia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nilipoyasikia maelezo hayo, nikapasua nguo zangu na koti langu, nikaongoa nywele zangu na ndevu zangu kwa huzuni kubwa na kuikaa chini na kufazaika.


Mordekayi alipojua yote yaliyotukia, akapasua nguo zake, akavaa nguo ya gunia, na kujitia majivu. Kisha, akapita katikati ya muji akilia kwa sauti ya uchungu.


Lakini, ingawa mufalme na watumishi wake wote waliyasikia maneno hayo yote, hawakuogopa wala kurarua nguo zao kwa huzuni.


Munapasua nguo zenu kwa kuonyesha huzuni, lakini inafaa mioyo yenu ipasuke vilevile. Murudilie Yawe, Mungu wenu. Yeye amejaa huruma na rehema, hakasiriki upesi, ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia zake kusudi asiazibu.


Mufalme wa Israeli aliposoma barua hii alipasua nguo yake na kusema: “Sababu gani mufalme wa Aramu anataka nimuponyeshe mutu huyu ukoma wake? Anafikiri kwamba mimi ni Mungu anayekuwa na uwezo wa kuua au kufufua? Mufahamu basi, muone kwamba mutu huyu anataka kuniletea ugomvi!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite