Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Yoane 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mutu asiyekuwa na upendo hamujui Mungu kwa maana Mungu ni upendo.

Gade chapit la Kopi




1 Yoane 4:8
14 Referans Kwoze  

Na sisi tumejua na kuamini upendo Mungu anaokuwa nao kwetu. Mungu ni upendo. Yule anayeishi katika upendo anaungana na Mungu, na Mungu anaungana naye.


Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma; wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.


Wapendwa wangu, tupendane, kwa maana upendo unatoka kwa Mungu. Kila mutu anayekuwa na upendo ni mutoto wa Mungu naye anamujua Mungu.


Basi kwa kumaliza, wandugu zangu, kwa heri. Mujikaze kuwa wakamilifu, mufarijiane ninyi kwa ninyi, mukuwe na nia moja, muishi katika amani, na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.


Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.


Lakini Mungu ni mwenye huruma nyingi. Alitupenda kwa upendo wake mukubwa;


Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kutoka kwa Yesu Kristo na kuitangaza kwenu: Mungu ni mwangaza, na ndani yake hamuna giza hata kidogo.


Basi kila mutu anayeungana naye hafanyi tena zambi; lakini kila mutu anayefanya zambi hakumwona wala kumujua.


Mutu anayesema kwamba anaishi katika mwangaza, lakini anamuchukia ndugu yake, yeye angali anaishi katika giza.


Mutu akijidai kwamba anamujua Mungu, lakini hashiki amri zake, yeye ni mwongo, nao ukweli hauko ndani yake.


kwa maana Mungu wetu ni kama moto wenye kuteketeza.


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite