Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Yoane 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Basi, kila mutu anayekuwa na tumaini hili katika Kristo anajisafisha mwenyewe kama vile Kristo anavyokuwa safi.

Gade chapit la Kopi




1 Yoane 3:3
21 Referans Kwoze  

Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


mutu yeyote anayesema kwamba anaungana na Mungu anapaswa kuishi sawa vile Yesu alivyoishi.


Kwa sababu hiyo, wapendwa wangu, mukiwa munangojea mambo yale, mufanye bidii apate kuwakuta safi bila kosa lolote na mukae na amani pamoja naye.


Basi mukuwe wakamilifu, kama vile Baba yenu wa mbinguni anavyokuwa mukamilifu.


Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Imani yenu na upendo wenu vinakuwa na musingi katika tumaini mulilowekewa mbinguni. Mulisikia juu ya tumaini lile mara ya kwanza wakati mulipohubiriwa ujumbe wa ukweli ni kusema Habari Njema.


Yeye hakufanya ubaguzi kati yetu na wao; ametakasa mioyo yao kwa sababu walimwamini.


Ilifanyika vile, kusudi kwa neema yake tupate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu na kuupata uzima wa milele tunaotumainia.


Kufuatana na hayo, ametupatia ahadi nzuri sana na kubwa mupate kuepuka uharibifu unaoletwa na tamaa mbaya za dunia na kushika hali yake ya kimungu.


Mukuwe wenye huruma, kama vile Baba yenu anavyokuwa mwenye huruma.


Hivi upendo umekamilishwa ndani yetu, kusudi tupate kuwa na tumaini kwa Siku ile ya hukumu. Kwa sababu maisha yetu katika dunia hii yanafanana na maisha ya Yesu Kristo.


Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.


Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatufariji kwa milele na kutupatia tumaini njema,


Isaya naye anasema: “Muzao wa Yese atatokea, atatawala watu wa mataifa, nao watamutumainia.”


bila kosa kwa wale ambao hawafanyi makosa, lakini mukali kwa waovu.


Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


Tumusifu Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kubwa ametupatia uzima mupya kwa njia ya kumufufua Yesu Kristo. Na kwa hiyo tumepata tumaini lenye uzima,


Na sawa vile Mungu aliyewaita ni mutakatifu, ninyi vilevile munapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite