Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Yoane 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Wapendwa wangu, sasa sisi ni watoto wa Mungu, wala namna tutakavyokuwa haijaonekana bado waziwazi. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwa sababu tutamwona vile anavyokuwa.

Gade chapit la Kopi




1 Yoane 3:2
37 Referans Kwoze  

Yeye atabadilisha huu mwili wetu wa uzaifu na kuufananisha na mwili wake wa utukufu kwa nguvu ambayo kwa njia yake anaweza kuwa na mamlaka juu ya vitu vyote.


Kristo ndiye uzima wenu wa kweli, naye atakapoonekana tena, basi ninyi mutaonekana pamoja naye katika utukufu wake.


Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.


Kwa maana wakati wa sasa tunaona kama mwenye kuangalia ndani ya kioo kisichoonyesha wazi, lakini wakati utakaokuja tutaona waziwazi. Kwa sasa ninajua tu mambo machache, lakini nyuma nitajua kwa utimilifu kama vile Mungu anavyonijua mimi.


Kwa maana wale Mungu aliowachagua tangu zamani, ndio aliofanya mupango juu yao tangu zamani, apate kuwafananisha na Mwana wake, kusudi Mwana wake akuwe muzaliwa wa kwanza wa wandugu wengi.


Lakini mimi nitauona uso wako, maana mimi ni mutu wa haki; nitakapoamuka nitajaa furaha kwa sababu unanitokea.


Na kama vile tulivyofanana na yule mutu aliyeumbwa kwa udongo, vilevile tutafanana na yule aliyetoka mbinguni.


Wataona uso wake na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao.


Kufuatana na hayo, ametupatia ahadi nzuri sana na kubwa mupate kuepuka uharibifu unaoletwa na tamaa mbaya za dunia na kushika hali yake ya kimungu.


Lakini ni kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mambo yale ambayo hakuna mutu aliyepata kuyaona wala kuyasikia, mambo yale ambayo hakuna mutu aliyepata kufikiri juu yake, ndiyo yale Mungu aliyowatayarishia wale wanaomupenda.”


Muangalie namna Baba alivyoonyesha upendo wake kwetu hata tupate kuitwa watoto wa Mungu! Na kwa hakika sisi ndio wao! Ndiyo maana watu wa dunia hawatutambui, kwa sababu hawakumujua Mungu.


Mungu alituma Roho wa Mwana wake ndani ya moyo wetu kwa kuhakikisha ya kuwa ninyi ni wana wake. Roho anayetuombea, akiita: “Baba!”


Ninaona kwamba mateso ya wakati huu wa sasa hayawezi kupima kulinganishwa na utukufu ambao Mungu atakaoonyesha kwetu waziwazi.


Kwa maana ninyi wote mumekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani na kuungana na Yesu Kristo.


“Baba, ninataka wale ulionipa wakuwe pamoja nami pahali nitakapokuwa, nao waone utukufu wangu, ndio ule utukufu ulionipa kwa sababu ulinipenda mbele ya kuumbwa kwa dunia.


Heri wale wanaokuwa na moyo safi, maana watamwona Mungu!


Na sasa watoto wangu, mukae ndani yake kusudi tukuwe na tumaini hakika wakati atakapotokea, na kutosikia haya mbele yake siku atakaporudi.


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


Kwa maana taabu tunayopata ni ndogo na ya muda tu, inatutayarishia utukufu mukubwa sana na wa milele unaokuwa muzuri zaidi kupita mateso haya.


Na nyuma ngozi yangu kuharibika hivyo, nitamwona Mungu nikiwa na mwili huu.


Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.


Funga midomo ya hao watu waongo, watu wenye kiburi na majivuno, ambao wanazarau watu wa haki.


nitamupatia nafasi ya ukumbusho na ya sifa katika nyumba yangu na kuta zangu, nafasi bora kuliko kuwa na wana na wabinti. Nitamupatia jina la kukumbukwa siku zote na ambalo halitafutwa hata kidogo.


Unanionyesha njia ya kufikia uzima. Kuwa mbele yako ni kujazwa furaha, kuwa kwa kuume kwako kunapendeza milele.


Lakini ni nani atakayevumilia siku ile atakapokuja? Ni nani atakayesimama kuvumilia atakapotokea? Yeye ni kama moto mukali unaosafisha chuma; ni kama sabuni ya mwenye kufua nguo.


Ni hivi itakavyokuwa siku ile Mwana wa Mutu atakayotokea.


Na zaidi ya ile hawataweza kufa tena, kwa sababu wataishi sawa vile wamalaika wanavyoishi. Nao watakuwa watoto wa Mungu, kwa sababu wamefufuliwa.


Lakini wamoja waliomupokea, ndio wale waliomwamini, aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu.


Na kufa kwake si kwa ajili ya taifa hili tu, lakini vilevile kwa ajili ya watoto wa Mungu waliosambazwa, kusudi apate kuwaunga katika umoja.)


Roho huyo mwenyewe anahakikisha ndani ya roho zetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu.


Viumbe vyote vinangojea kwa hamu sana wakati Mungu atakapowaonyesha watoto wake waziwazi.


Wapenzi, siwaandikii amri mupya, lakini ile ya zamani muliyoijua tangia mbele. Na amri hiyo ya zamani ni lile neno mulilosikia.


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Wapendwa wangu, zamiri yetu isipotuhukumu, sisi tuko na tumaini mbele ya Mungu.


akiwa na uwezo sawa ule uliopewa na Baba yangu. Na zaidi ya ile nitamupa nyota ya asubui.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite