Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Yoane 2:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mutu anayesema kwamba anaishi katika mwangaza, lakini anamuchukia ndugu yake, yeye angali anaishi katika giza.

Gade chapit la Kopi




1 Yoane 2:9
14 Referans Kwoze  

Kama mutu akisema “Ninamupenda Mungu,” naye anamuchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana yule asiyemupenda ndugu yake anayemwona, hawezi kumupenda Mungu asiyemwona.


Lakini anayemuchukia ndugu yake anaishi na kutembea katika giza, wala hajui pahali anapokwenda kwa sababu giza limemupofusha macho.


“Lakini ninyi hamujui wala hamufahamu! Ninyi munatembea katika giza la upotovu! Misingi yote ya haki katika dunia imetikiswa!


Lakini mutu asiyekuwa na tabia hizo ni kipofu, hawezi kuona. Yeye amesahau kwamba amekwisha kutakaswa zambi zake za zamani.


Mutu akijidai kwamba anamujua Mungu, lakini hashiki amri zake, yeye ni mwongo, nao ukweli hauko ndani yake.


Tukisema kwamba tunashirikiana naye, lakini tunaishi katika giza, tunasema uongo, nayo matendo yetu si ya kweli.


Yesu akawajibu: “Mungekuwa vipofu, hamungekuwa na zambi. Lakini kwa maana munajidai kwamba munaona, mungali katika zambi.”


Usimuchukie ndugu yako ndani ya moyo wako, lakini upatane siku zote na mwenzako kusudi usitende zambi.


Abusaloma alimuchukia Amunoni sana hata hakusema naye, kwa sababu alimukamata dada yake Tamari kwa kinguvu, akalala naye.


Katika siku zile, kulikuwa mukutano wa wandugu waamini yapata watu mia moja makumi mbili. Basi Petro akasimama katikati yao, akasema:


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite